Wednesday, September 28, 2016

NJIA ZA KUKUSAIDIA KATIKA KUFIKIA MALENGO YAKO

Habari za Leo ndg yangu,rafiki zangu,kaka zangu ,Dada zangu,karibun sana katika kuendelea kushauriana na kupambanua mambo yaliyo muhimu katika malengo ya maisha yetu.
   Siku ya Leo napenda tuangalie ya kwamba ni namna gan utafikaia malengo yako endapo utatumia baadhi ya njia kama zifuatazo
Cha kwanza inabid tutambue maana ya vitu vifuatavyo ambavyo ndivyo vitu muhimu kukufikishia lengo lako.
  1:Ndoto
Hii ni fikra au maono ambayo mtu humjia kichwan mwake kutokana na vile vitu apendavyo viweze kutokea maisha yake.ambapo hii ndio njia ya kwanza muhimu ambayo ukiweza kuwa na ndoto ya kuweza kufanya kitu fulani na kukifanikisha huwa na mafanikio yaliyokuwa kuwa tayar umeyapanga kichwan mwake.
   2:Malengo
Hii ni njia nyingin ambayo kutokana na ndoto yako huja kutengeneza kutengeneza malengo.ambapo haya malengo huwa ni ndoto ambayo mtu hujipangia ya kwamba katika kufanikisha i nabidi nitumie muda gan na vitu gan katika kufikia lengo
  3:Mikakati
Hii ni mipango ambayo mtu hujiwekea katika ndoto zake na malengo yake ambapo i nabidi tutafakari ya kwamba katika Mikakati yangu ya kufanukisha hili i nabidi nianze na kipi na nimalizie kipi ili pale uanzapo usiweze kupata shida.
4:Action/vitendo
Sasa hapa ndipo ufanikishapo lengo lako kutokea katika ndoto mpaka vitendo na ndipo ufanyapo na utekelezspo ndoto zako kupata
mafanikio .

    Ndoto
        ⬇     
   
   Malengo
         ⬇
  Mikakati
         ⬇
  Action(vitendo )   
KATIKA vitendo ndio sehemu ambapo utavifanyia kazi vile vyote ulivyojifunza kwa nadharia na kufanya kwa vitendo zaid.
   Lakn pia katika hivyo vilivyopo hapo juu inatakiwa uweze kujiwekea
   1:muda
Hapa unajipangia ni kwa muda gani niwe nimefanikisha lengo au mafanikio yangu
2;kipimo
Hapa unajiwekea kipimo ya kwamba kufikia muda fulani nitakuwa nimefanikisha lengo Lang kwa kipimo cha asilimia kadhaa na baadae kias kadhaa
3;level utakayo
Sasa hapa unaangalia je katika maisha yangu yahitajika niwe level ya aina gan.mfano kama una lengo la kuwa mfanyabiashara  je unataka uwe wa level ya kimkoa kitaifa au kimataifa .
   KATIKA maisha ya mafanikio hivyo vitu vyahitajika sana uvitambue .
     Nakutakia siku njema na majukum Mema katika kufikia nia na malengo yetu
MUNGU yu pamoja nasi usikate Tamaa mtegemee MUNGU kila siku ianzapo na iishapo kwa maana ni rehema na neema zake tu.
  Phone 0755778896
Email:barakaasajilemwakyoma@gmail.com

No comments:

Post a Comment