Thursday, March 30, 2017

ONDOA SUMU MWILINI KWA NJIA zifuatazo

Mwili unaweza kupatwa na sumu au takataka zisizohitajika na mwili kwa namna mbili, ama kupitia mazingira tunayoishi (viwanda, migodi nk) au kupitia vyakula na vinywaji ambavyo tunatumia kila siku. Sumu au taka pia zinaweza kuingia mwilini kupitia dawa mbalimbali hasa za kizungu tunazotumia kujitibia magonjwa mbalimbali.

Mwili huzalisha hizi sumu au takataka (free radicals) kila mara kunapofanyika mmeng'enyo wa chakula mwilini mwako.

Ishara zitakazokuonyesha mwili wako una sumu nyingi:

-Uchovu sugu
-Maumivu ya maungio
-Msongamano puani
-Kuumwa kichwa kila mara
-Tumbo kujaa gesi
-Kufunga choo au kupata choo kigumu
-Kukosa utulivu
-Matatizo mbalimbali ya ngozi ikiwemo chunusi
-Pumzi mbaya
-Mzunguko wa hedhi usio sawa
-Kuishiwa nguvu
-Kushindwa kupungua uzito
-Kupenda kula kula kila mara

Njia 16 za kuondoa sumu mbalimbali mwilini

1. Fanya mlo wako mmoja wa siku kuwa ni matunda pekee

Amua moja ya mlo wako kwa siku uwe ni matunda pekee bila chakula kingine zaidi. Unaweza kuamua ama chakula cha asubuhi au cha jioni kuwa ni matunda pekee, ndiyo kwenye sahani yako unajaza matunda tu mbalimbali sahani ijae na ule hayo tu kama ndiyo mlo wako ukimaliza unaweza kunywa juisi ya matunda au maji pekee.

2. Kula vyakula vya asili zaidi kuliko vya viwandani

Kama unataka kuepuka sumu au takataka nyingine kirahisi kuingia katika mwili wako basi pendelea zaidi kula vyakula vya asili vinavyopikwa nyumbani kuliko kula vya kwenye makopo au vya dukani  au vya kwenye migahawa (fast foods).

3. Fanya masaji

Kwa bahati mbaya waTanzania wengi hawajuwi kuwa masaji ni sehemu ya tiba au ni dawa pia kwa magonjwa mengine mengi mwilini. Wengi tunaichukulia masaji kama kitu cha starehe tu (relaxation) lakini unaweza kutumia masaji kama njia mojawapo ya kuondoa sumu mwilini na utafanikiwa kwa muda mfupi sana.

4. Kunywa maji mengi kila siku

Sababu kubwa ya watu wengi kutengeneza sumu au taka mwilini mwao ni kutokunywa maji mengi kila siku. Maji ni uhai, bila kunywa maji mengi kila siku ni sawa na kwenda dukani bila hela mfukoni. Haijalishi upo mazingira gani kama ni ya baridi au ni ya joto ni LAZIMA UNYWE MAJI YA KUTOSHA KILA SIKU IENDAYO KWA MUNGU.

Unahitaji maji glasi 8 mpaka 10 kila siku. Watu wengi wanahangaika namna ya kuondoa sumu kusafisha miili yao bila kujua kuwa maji pekee ya kunywa yanatosha kwa kazi hiyo. Kumbuka asilimia 94 ya damu yako ni maji, asilimia 85 za ubongo wako ni maji, hivyo ili kusafisha damu na mwili kwa ujumla ni lazima unywe maji ya kutosha kila siku.

5. Acha chai ya rangi na Kahawa

Kama tayari imethibitika una sumu au takataka nyingi mwilini nakushauri uache kunywa chai ya rangi na kahawa. Badala yake hamia kutumia chai yenye tangawizi au mdalasini au mchaichai. Chai ya rangi na kahawa vina kaffeina ambayo kwanza huyasukuma maji nje ya mwili kwa haraka na kuuacha mwili bila kuwa na maji ya kutosha kwa ajili ya kazi zake. Kaffeina pia ni madawa ya kulevya kundi la madawa yanayosisimua mwili (stimulants drugs).

6. Fanya mazoezi ya viungo

Inashangaza sana kuona waTanzania wengi hawaoni umhimu wa kufanya mazoezi ya viungo. Mazoezi ya viungo ni jambo la lazima kama ilivyo chakula. Iwe unaumwa au huumwi, iwe una uzito kuzidi au una uzito wa kawaida hakikisha unapata muda wa kufanya mazoezi.

Mazoezi yanakusaidia kukufanya ujisikie vizuri na hivyo kukuondolea mfadhaiko au stress kirahisi zaidi, sambamba na hilo mazoezi ni dawa tosha na nzuri ya kuondoa sumu mwilini haraka zaidi. Hakikisha jasho linakutoka la kutosha na iwe ni jambo la kila mara na siyo unaenda jumamosi na jumapili (weekend) tu, hiyo haitoshi, fanya mazoezi mara 4 mpaka mara 5 kwa wiki.

7. Kula zaidi vyakula vyenye nyuzinyuzi (faiba)

Umesikia mara nyingi kwamba unahitaji kula zaidi vyakula vyenye nyuzinyuzi kwa ajili ya kuwa na afya bora, mmeng’enyo wa chakula wenye afya na hata kukusaidia kupunguza uzito. Kile ulikuwa hujuwi pengine mpaka sasa ni kuwa vyakula hivi vyenye nyuzinyuzi ni vizuri pia katika kusafisha mwili na kuondoa sumu au takataka mbalimbali.

Vyakula vyenye nyuzinyuzi nyingi ni pamoja na parachichi, ndizi, peazi, karoti, pilipili hoho, mchele wa brown (ule wanashauriwa watu wa kisukari wautumie), maharage meusi, njegele, tende, viazi vitamu, tufaa (apple), machungwa, ugali wa dona pia mkate wa unga wa ngano ambao haujakobolewa.

8. Funga kula

Ndiyo, kama ulikuwa hujuwi namna nyingine rahisi ya kuondoa au kupunguza sumu mwilini ni kufunga kula kabisa kutwa nzima. Ukifunga kula mwili unalazimika kuvitumia vile vilivyomo ndani yake bila kushughulika kuvisaga vingine vipya unavyokula. Kunapokuwa hakuna shughuli ya kuvisaga na kumeng'enya chakula kipya mwilini ndipo mwili unaweza kuondoa sumu na taka nyingine kirahisi zaidi.

Amua kufunga kula kabisa kwa wiki mara 2 hata 3 ili kuondoa au kupunguza sumu, hii inaweza kuwa pia ni njia mojawapo ya kufanya maombi na kujiweka karibu na muumba wako.

TABIA ZA BLOOD GROUP B

Muendelezo.....wa blood group kama ifuatavyo...

Blood group"undefined"

Nb:...Hawa watu huwa Tabia zao hazielewek wanatabia yakubadilika badilika kama kinyonga na ngumu sana kuish na MTU.

Blood group B..."balanced ".
1=ma MC wengi wapo group B.

2= Wasanii/waimba.

3=Waongeaj sana.

Nb:...hawa watu Mara nying huwa wanaweza kuish na MTU yeyote kutokokana aina ya blood Group.

Wednesday, March 29, 2017

TAMBUA TABIA ZA BLOOD GROUP A

Habar ya mda huu,

Leo tujifunze kuhusu Tabia na aina ya Damu group A.

1=Tabia ya watu wenye group A huwa ni wabinafs sana,Anaweza akawa anafaham kitu lakin kakaa nacho tuu na asimshirikishe MTU yaan ni wabinafs sana.

2=Wapole,Na kutokana na hii hali au aina ya group LA dam huwapelekea kuwa na hasira sana na hasira zao huwa haziish yaan ( kinyongo).mnaweza kugombana Leo ukamuomba msamaha baada ya mwaka moja akaja kukukumbusha kuwa kuna siku ulimfanyia kitu fulan,huwa hawasahau.

3=Wanafata sana sheria.

4=wanapenda sana details,kwa mfano watu wenye group A unaweza kumtuma Dukan ukamwandikia kwenye karatas anunue hiki na hiki lakin akifika Dukan anaweza tena kukupigia hivi ulisemaje ni nunue ni Na nin.

5=Hawapend shida.

Sasa changamoto inakuja huyu MTU mwenye group A anapokutana na MTU Wa group 0 huwa shida sana,kwasababu group A ni Wapole wanapenda kuelekezwa kimoja kimoja wakati group 0 huwa ni wababe sana na huwa hawapend kurudia rudia vitu,akishasema amesema.

Kwa hiyo ukiangalia hata kwenye mahusiano MTU Wa Group A ni ngumu sana kuish na group 0.MTU mwenye group O hakawii kukwambia usinisumbue,acha yaan huwa hawapend usumbufu usumbufu hasa wanapokutana na group A.

Monday, March 27, 2017

MADHARA YA POMBE KIAFYA

Pombe za aina ya kinywaji ambacho kinapendwa sana katika jamii, hata hivyo licha ya kuwepo kwa taarifa ya kwamba pombe huongeza furaha ya moyo,  na kuzuia matatizo yatokanayo na msongo wa mawazo, tafiti mbalimbali zinasema ya kwamba pombe zina aina zote kemikali ambazo baadhi ya hizo kemikali huwa ni katika mwili wa mwanadamu.

Labda kwa dakika chache tuangalie matatizo yatokanayo na utumiaji wa pombe.

1;Vidonda vya tumbo.
2;Kansa ya utumbo.
3;Kusinyaa kwa Ini.
4;Kansa ya Ini.
5;Kansa ya umio(oesophagus)
6;Vindonda kwenye mapafu.
7;Utapiamlo hasa wale wanaokunywa huku lishe duni
.Matatizo ya ganzi miguuni na mikononi(Peripheral Neuropathy).
8.Kisukari.
9;Figo kushindwa kufanya kazi.(Renal failure)
10;Kansa ya figoKukosa au upungufu wa hamu ya tendo la ndoa.
(Loss of Libido)
12;Upungufu wa nguvu za kiume.
           Kuongeza kasi kwa baadhi ya magonjwa hata kama unatumia dawa kama vile Kifua Kikuu,
   1;Kansa,
    2;KisUkari,
     3;Shinikizo la damu la kupanda.
    3;Kukosa hamu ya kula.
(Anorexia)
4; Kutovyonzwa vyema kwa chakula(Malabosorption)
Ugonjwa wa kongosho.(Pancreatis).
          Kichaa cha pombe(mtu hawezi kufanya kazi bila ya pombe,au anakuwa kama mgonjwa lakini akipewa pombe tu anakuwa mzima)
Jambo la muhimu ni kuhakikisha unaepuka utumiaji wa pombe ila kuepuka matatizo niliyoyatabainisha hapo awali.

HISTORIA YA CHIFU WA WAHEHE MKWAWA 1

Mkwawa alikuwa chifu wa wahehe na kiongozi mkuu wa kabila la wahehe ambaye alizaliwa mwaka 1855 -1898 katika kijiji cha Lungemba mkoani Iringa. 

Baba yake mzazi ni Mzee Munyigumba.Baada ya kuzaliwa Mkwawa alipewa jina la 'Ndasalasa' yaani ikiwa na maana ya kupapasa papasa. Alipoofikisha umri wa miaka 23 ulitokea uvamizi ambapo baba yake mzazi Mzee Munyigumba alivamiwa na Wangoni.

Baada ya kuvamiwa Mzee Munyigumba alikimbilia mlima wa Nyamulenge. Alipokuwa pale mlimani Wangoni walimzingira kila pande hivyo Mzee Munyigumba aliamua kuingia pangoni, baada ya kuingia pangoni Wangoni waliamua kuchoma moto pale pangoni ili basi Mzee Munyigumba afie ndani ya pangoni lakini mpango wao haukutimia kwani Mkwawa aliwahi kumuokoa baba yake. 

Mzee Munyigumba alimsifu sana mtoto wake kwa ushujaa alioufanya wa kumkomboa hivyo alimtunuku jina la kishujaa yaani aliitwa "Mkwava Mkwavinyika".

Mapigano kati Mkwawa akiwa na wafuasi wake wa kabila la Wahehe dhidi ya Wangoni yalipamba moto sehemu ya Makambako ambapo Wangoni walishindwa na kuamua kukimbia.

Licha ya Wahehe kushinda lakini bado waliwasifu Wangoni kwa mapigano waliyoyaonesha wakisema kuwa " Leo tumekutana na Makambako" ikiwa na maana kuwa wamekutana na madume hivyo sehemu hiyo tangu siku hiyo ikawa inaitwa Makambako mpaka leo hii.

Lakini baada ya kumaliza mapigano dhidi ya Wangoni, Mkwawa na kikosi chake walirudi Iringa mjini. Kwa bahati mbaya alisikia taarifa mbaya kwamba baba yake amefariki hivyo ilibidi baba yao mdogo Mzee Mwaije agawanye nchi ambapo upande wa kusini alipewa Mkwawa na upande wa kasikazini alipewa Muhenga. Baada ya kupewa maeneo hayo Shemeji yao Mwambambe mwalinyungu ambaye asili yake ni mtu wa Tabora aliwagombanisha Mkwawa na Muhenga. 

Mwambambe alifika Iringa wakati akiwa Mdogo sana hivyo baba yake Mkwawa alikuwa akimtumia kwenda kuchukua dawa za kichifu na dawa za kivita wakati wakiwa njiani pale walipotokea maadui Mwambambe alikuwa na nguvu za ajabu alikuwa na uwezo wa kumkamata adui mmoja kila upande na kuwagonisha vichwa mpaka wanafariki hivyo baba yake Mkwawa pamoja na wahehe wote kiujumla walimpenda sana Mwambambe kufuatia sifa hizo Mzee Munyigumba alimpatia binti yake amuoe. Hivyo Mwambambe aliwagombanisha Mkwawa na Muhenga kwa kumwambia Muhenga kwamba amepata eneo dogo kuliko Mkwawa hivyo alimwambia kuwa yeye yupo tayari kumsaidia ili apate eneo kubwa.

Wakaanzisha vita ya kumpiga Mkwawa hivyo Mkwawa alitoroka kuelekea Dodoma, wakati akiwa huko baba yake Mdogo aliyekuwa akiishi huko alimuuliza kuwa nchi kamuachia nani? Ilibidi Mkwawa amueleze kilichotokea na kumalizia kwamba amemuachia Mdogo, hapo ndipo baba yake Mdogo alipomwambia inabidi arudi Iringa kwa ajili ya kupambana kwani yule Mdogo wake pia anaweza kupigwa na Mwambambe akachukua nchi na Mwambambe asili yake ni mtu wa Tabora hivyo nchi itakuwa ya watu wa Tabora.

Basi ilibidi Mkwawa arudi Iringa kupambana na hao ndugu zake. Lakini kwa bahati mbaya hawa ndugu zake walishasababisha mauaji, walishinikiza mpaka mama yake Mkwawa alijiua. Baada ya Mkwawa kukimbilia Dodoma walimkamata mama yake na kumlazimisha awaoneshe dawa ya uchifu ambayo ilikuwa inaitwa "LIHOMEO" baada ya kuwa amelazimishwa sana mama Mkwawa aliamua kuwaambia kuwa dawa hiyo inapatikana sehemu inayoitwa Kikongoma hivyo waliondoka kuelekea huko Kikongoma kuchukua dawa. Walipofika Kikongoma walienda mpaka kwenye daraja la Mungu baada ya kufika hapo mama Mkwawa aliwaambia kuwa "Nimefika sehemu ilipo dawa lakini mashariti yake ni lazima nivue nguo ndipo niweze kuichukua hiyo dawa, sasa nyinyi ni wanangu nitavuaje nguo mbele yenu?" Hivyo wale jamaa ilibidi wawatume wamama wawili waende naye wao wenyewe walibaki nyuma kidogo.

Mama Mkwawa alisogea hadi karibu na daraja la Mungu sehemu ambapo kulikuwa na jiwe kubwa, mama mkwawa alivua nguo zake zote na kuziweka juu ya lile jiwe kisha akaanza kulizinguka lile jiwe Mara kadhaa halafu akajirusha ndani ya maji huku akisema, "Mwambambe ulitaka nikuoneshe dawa ili umuue mwanangu umenikosa". Alizungumza kwa lugha ya kihehe kisha akajirusha ndani ya ule mto.

Sunday, March 26, 2017

CHAKULA MUHIMU KWA MJAMZITO

Kwa ajili ya afya ya mama na mtoto ni muhimu sana mwanamke apate chakula bora. Ukosekanaji wa chakula bora kunaweza kukasababisha mtoto kuzaliwa kabla ya mda wake au na uzito mdogo ambao unaweza ukachangia katika kuzuia ukuaji wa ubongo na mwili kwa ujumla.

Na endapo mama mjamzito atakosa mlo bora uliombatana na protini anaweza akapata anaemia, infection, matatizo katika placenta, matatizo katika labor, c-section(kuzaa kwa upasuaji wakati wa kujifungua), kutokupona kwa haraka, matatizo katika kunyonyesha, toxemia na pre-eclempisa(haya ni magonjwa yanayosababishwa na maini kutoweza kufanya kazi yake vizuri

Hivyo ili kujenga afya ya mama na mtoto imeshauriwa ya kwamba mama mjamzito anatakiwa apate 100 grams za protein kwa siku.

Ifuatayo ni mlo kamili anaotakiwa apate mama mjamzito kila siku ya ili kuweza kupata afya bora:

1.Maziwa na vyakula vya jamii ya maziwa:
Glasi nne au zaidi ya maziwa ya aina yoyote pamoja na/au vyakula vyenye jamii ya maziwa kama jibini, mtindi,siagi, ice cream. Maziwa ni muhimu kwa protein, calcium, vitamins na virutubisho vingi. Vitasaidia ukuaji wa mifupa, misuli na nerves. Ni muhimu kwa damu yenye afya, kusaidia usingizi na kusawazisha mapigo ya moyo.

Mayai:
Mayai mawili kwa siku husaidia kuupa mwili protein, vitamins minerals na vitamin A ambayo itasaidia kuzuia infections.

Vyakula vyenye Protein
Serving mbili ya samaki, maini , kuku, nyama ya ngombe, mbuzi, kondoo au nguruwe, maharagwe au jibini. Kusaidia ujengaji mifupa, meno, misuli, ubongo na mwili kwa ujumla. Ukosekanaji wa protein ya kutosha kutasababisha kuchoka, uvimbe na kutojisikia kula au appetite ndogo.

Mboga za majani.
Spinach, cabbage, collard greends, mchicha, matembele. Mboga hizi ziwe fresh na zile zenye rangi ya kijani iliyokolea(hizi ndio zenye virutubisho vya kutosha).  Mboga hizi zitakupa Vitamin A na B, pia virutubisho vitakavyosaidia mwili kuabsorb protein ya kutosha, ukuaji wa mwili, na utengenezaji wa damu. Kutopata mboga za kutosha kunaweza sababisha mama kupata anemia.

Vyakula vyenye vitamin C.
Kipande kimoja au viwili vya machungwa au juisi ya ndimu, machungwa, nyanya. Vitamin C itasaidia uterus kuwa na nguvu ya kutosha ili kufanya kazi vizuri wakati wa labor, pia itasaidia kulinda mwili na infection na kusaidia kuabsorb iron kwenye mwili.

Maji ya kunywa.
Kunywa maji mengi ya kutosha. Maji huchangia kwa asilimia 75 ya uzito wa mtoto wako atakapozaliwa. Usipopata maji ya kutosha utaishiwa na nguvu kwa asilimia 20 na kupata matatizo ya dehydration na kichwa kuuma.

Tumia chumvi kiasi.
Chumvi  kusaidia kuzunguka kwa damu kutoka mwilini kwenda kwenye placenta. Kutopata chumvi ya kutosha kunaweza kusababisha miguu kuuma na uchovu.

Kwenye sehemu ya pili tutaongelea virutubisho kadhaa na umuhimu wake kwa mama mjamzito na mtoto. Ila kumbuka utumiaji wa chumvi kwa wingi una madhara kiafya.

Saturday, March 25, 2017

FAIDA Za TUNDA LA STAFELY

1.  Majani yake hutumika kama chai na kutibu kuharisha damu, mafua na husaidia mfumo wa umeng'enyaji  wa chakula.

2.  Mizizi yake huua minyoo kwa aina zake .

3.  Mbegu hutengenezwa dawa ya kula na kufukuza wadudu waharibifu.

4.  Tunda ni chanzo kikuu cha  vitamin C , Iron, Niacin Riboflavin na asilimia 12% ya tunda hili ni sukari salama.

5.  Tunda hili pia ni chakula,unaweza kutengeneza juice tamu kwa familia .

Ushauri 
Mgonjwa wa saratani anapokuwa kwenye Tiba ya hospitali anashauriwa pia kula sana Stafeli ili kumpunguzia makali ya dawa za Saratani pamoja na kupunguza maumivu.
Tukumbuke maumivu ya saratani ni maumivu makali kuliko na wagonjwa wanapewa zile dawa kali sana  za maumivu.
Matumizi ya tunda hili yatampunguzia mgonjwa madhara ya dawa.

Kwanini usilifanye tunda hili kuwa Rafiki kwako na familia yako?
Nashauri kila mmoja wetu apande mti japo mmoja wa tunda hili  nakujipatia faida bila kutumia gharama kubwa ya kununulia, Miili yetu inahitaji tunda hili kwa wingi.

Stafeli majina yake mengine ni  Soursop au Graviola.

FAIDA Za TUNDA LA STAFELY

1.  Majani yake hutumika kama chai na kutibu kuharisha damu, mafua na husaidia mfumo wa umeng'enyaji  wa chakula.

2.  Mizizi yake huua minyoo kwa aina zake .

3.  Mbegu hutengenezwa dawa ya kula na kufukuza wadudu waharibifu.

4.  Tunda ni chanzo kikuu cha  vitamin C , Iron, Niacin Riboflavin na asilimia 12% ya tunda hili ni sukari salama.

5.  Tunda hili pia ni chakula,unaweza kutengeneza juice tamu kwa familia .

Ushauri 
Mgonjwa wa saratani anapokuwa kwenye Tiba ya hospitali anashauriwa pia kula sana Stafeli ili kumpunguzia makali ya dawa za Saratani pamoja na kupunguza maumivu.
Tukumbuke maumivu ya saratani ni maumivu makali kuliko na wagonjwa wanapewa zile dawa kali sana  za maumivu.
Matumizi ya tunda hili yatampunguzia mgonjwa madhara ya dawa.

Kwanini usilifanye tunda hili kuwa Rafiki kwako na familia yako?
Nashauri kila mmoja wetu apande mti japo mmoja wa tunda hili  nakujipatia faida bila kutumia gharama kubwa ya kununulia, Miili yetu inahitaji tunda hili kwa wingi.

Stafeli majina yake mengine ni  Soursop au Graviola.

Friday, March 24, 2017

TIBA TOSHA YA MBEGU ZA MABOGA

Watu wengi hupenda zaidi ya kula boga kuliko mbegu zake. Wengi hufanya hivi kwa sababu huona hazina faida kwa kuwa wanavutiwa na boga zaidi, hii sawa nakusema watu hupenda zaidi mnofu kuliko kula mifupa, lakini ukweli ni kwamba mbegu za maboga ni za muhimu sana kwani zina wingi protini na madini ya kutosha ambayo ni muhimu sana katika miili yetu.

Madini ambayo yanapatikana katika mbegu za maboga kama vile zinki, kopa, maginizia, manganizi na chuma. Tafiti mbalimbali zimethibitisha pasipo na shaka kuwa mbegu za maboga zina faida nyingi kiafya na zina uwezo wa kukuepusha na magonjwa hatari zaidi ya 10  na magonjwa hayo ni kama:

1.Magonjwa ya moyo.
Kiasi kingi cha madini ya magnesium katika mbegu za maboga yanazifanya mbegu hizi kuwa muhimu sana kwa watu wenye magonjwa mbalimabli ya moyo. Madini ya magnesium ni muhimu kwa ajili ya kuimarisha msukumo wa damu kwenye moyo na kuimarisha afya ya mishipa ya damu hatimaye kutibu na kuzuia magonjwa ya moyo.

2. Husaidia uzalishaji wa maziwa kwa wingi kwa kina mama wanaonyonyesha.
Hivyo kwa mama anenyonyesha anashauriwa kutumia  mbegu za maboga kwa wingi ili kuzalisha maziwa kwa wingi.

3. Huongeza uwezo wa macho kuuona vizuri.
Mbegu za maboga zina Vitamini E, vitamini A, lutein, beta-carotene na zeaxanthin, vitu hivi vinavyopatikana katika mbegu za maboga ni mhimu kwa ajili ya nuru ya macho. Vitamini A na madini ya zinki ni mhimu kwa ajili ya uzalishaji wa ‘melanin’ kimeng’enya mhimu ambacho hutengenezwa kwa asili na miili yetu kwa ajili ya ulinzi wa afya ya macho.

4.Husaidia kuondokana na matatizo ya unene unaotokana na wingi wa mafuta ( cholestrol) mwilini.

5.huondoa harufu mbaya ya kinywa na husaidia pia wenye tatizo la kufunga choo au kupata choo

6.Husaidia kurekebisha sukari mwilini na kuwezesha kongosho kufanya kazi yake vizuri.

7. Huondoa sumu mbalimbali mwilini na hasa kwenye figo.

8.Husaidia kuondoa shinikizo la damu.

9. Ni kinga dhidi ya kansa ya kizazi kwa wanaume na wanawake.

10. Huboresha akili na kumbukumbu kwa watoto na watu wazima ( kazi ya zinc na omega 3 Fatty).

Hivyo kila wakati inashauriwa kutafuna mbegu hizi zikiwa mbichi kuliko zikiwa zimechemshwa au kukaangwa,  kwani ukitumia ambazo zimechemshwa au kukaangwa kuna uwezekano mkubwa wa kupoteza baadhi ya vitamini.

Thursday, March 23, 2017

Fursa zituzungukazo

1. Kununua Mashine za kukoroga zege na kukodisha.
2. Kununua Mashine za kukata vyuma na kuzikodisha.
3. Kutengeneza na kuuza tofali
4. Ufundi, Website updating/Database: Katika Halmashauri, Manispaa, Mashule, Wizara, Wilaya na           Makampuni mbalimbali.
5.  Kuanzisha kituo cha redio na televisheni
6. Kufunga na kutengeneza vifaa mbalimbali vya electroniki na mawasiliano mfano; compyuta na vifaa       vya compyuta na mawasiliano.
7. Kuuza software; mfano Antivirus, Operating Systems, Pastel, Tally, Myob, n.k
8. Kushona na kuuza nguo.
9. Kufungua Duka la kuuza nguo mpya; suit, socks, batiki, nguo za asili, Mashuka, Mashati, Suruali,
10. Ufugaji wa mifugo mbalimbali mfano Kondoo, Mbuzi, Ng’ombe, Kuku, Bata, na wengine.
11. Kufungua stationery, kuuza (supply) vitabu na vifaa mbalimbali ktk mashule na vyuo.
12. Kutoa ushauri mbalimbali wa Kitaalamu.
13. Kuuza viazi, mahindi, mihogo, kutengeneza popcorn na kuziuza.
14. Kusajili namba za simu na kuuza vocha
15. Kuwa na mradi wa Pikipiki zisizotumia mafuta na zinazotumia mafuta
16. Kilimo cha mazao mbalimbali kulingana na hali ya hewa ya sehemu husika.
17. Kuuza Mitumba
18. Kusimamia miradi mbalimbali
19. Kufungua duka la kuuza mitambo mbalimbali
20. Kufungua banda la chakula na chips
21. Kukodisha turubai viti na meza
22. Kufungua Supermarket
23. Kufungua Saluni
24. Kufungua Bucha
25. Video Shooting & Editing.
26. Kufungua Internet cafe
27. Duka la kuuza matunda
28. Kufungua duka la kuuza vifaa vya simu za mkononi na landline.
29. Kufungua duka la vifaa vya ujenzi; cement, vifaa vya umeme, duka la mabati
30. Kutengeneza michoro mbalimbali ya majumba na miradi ya ICT
31. Kuchapa vitabu, bronchures, n.k
32. Kuanzisha kampuni ya ujenzi (Building contractor)
33. Kuuza Vifaa vya umeme wa nishati ya jua (solar) ,battery, inverter na vifaa vingine vya solar n.k
34. Kuuza maji kwa jumla na rejaleja.
35. Kutengeneza na kuuza Unga wa lishe bora.
36. Kukodisha Music
37. Kuanzisha Mradi wa Taxi
38. Kuanzisha mradi wa Daladala
39. Kuuza vifaa vya Kompyuta, laptops, converters, HDDs, Monitors, Softwares, CD Copiers na vifaa           vingine.
40. Kununua magenerator na kukodisha
41. Kufungua kampuni ya kutoa huduma za simu
42. Kufungua kampuni ya kutoa huduma za internet (ISP)
43. Kuuza mabati na vigae
44. Kujenga apartments
45. Kufungua Kisima cha mafuta ya taa au mafuta ya aina zote
46. Kufungua Duka la samaki
47. Kufungua Duka la nafaka
48. Kufungua Shule za Awali, Shule za Msingi, Sekondari na Vyuo.
49. Kujenga hostel
50. Kuuza vocha na ving’amuzi vya DStv, Zuku, Startimes, Easy TV, TNG, Digitech, Continental.
51. Kujenga mtambo wa kuzalisha umeme na kuuza katika viwanda na wananchi.
52. Ufundi simu
53. Kufungua Hospitali, Zahanati.
54. Maabara ya Macho, Meno
55. Kuchimba/Kuuza Madini
56. Kufungua ofisi ya kutoa huduma ya simu na fax
57. Kuuza miti na mbao
58. Kufungua Grocery, bar
59. Kufungua studio ya kupiga na kusafisha picha
60. Kucharge simu/battery
61. Duka la TV na vifaa vingine
62. Kuanzisha biashara ya kuuza vyakula katika sherehe na tamasha mbalimbali (catering).
63. Banda la kupigisha simu
64. Kuuza na kushona Uniform za shule
65. Kuanzisha duka la kuuza vitu kwa jumla.
66. Kufungua gereji za kutengeneza bajaji, pikipiki na magari
67. Kuuza vyuma, pembejeo, rake, jembe
68. Kuuza fanicha
69. Kufungua sehemu ya kuziba pancha za matairi
       ya magari na mitambo.
70. Kujenga nyumba za kulala wageni (hotel)
71. Kuagiza na kuuza vifaa vya aluminium.
72. Kuuza vioo
73. Kushona na kukodisha nguo za harusi
74. Kufungua yard kwa ajili ya kuosha magari
75. Kuuza mashine za kuchomelea (welding machine).
76. Kuuza vifaa vya kuvaa Site (boots, helmets etc)
77. Kununua mabasi kwa ajili ya kusafirisha wanafunzi
78. Kufungua studio ya kutengeneza vipindi vya redio na televisheni
79. Kuanzisha ofisi ya michezo ya televisheni (TV Games)
80. Kufungua benki
81. Kuwa na malori ya kubeba kokoto na mchanga
82. Kuuza vifaa mfano TV, CCTV Camera, n.k
83. Kuwa dalali wa vitu mbalimbali
84. Kuanzisha mradi wa kukodisha fork lift na winchi (crane)
85. Kuanzisha kiwanda cha kutengeneza viatu.
86. Kuanzisha viwanda mbalimbali
87. Duka la vifaa vya simu na gadgets mbalimbali zinazoendana na mawasiliano ya Vodacom, TTCL,          AIRTEL, TIGO, ZANTEL, n.k.
88. Kujenga Ukumbi wa kukodisha kwa sherehe, mikutano mbalimbali
89. Kununua matrekta, mitambo ya ujenzi wa barabara na kukodisha
90. Kutengeneza antenna na kuuza
91. Kufungua mradi wa Machine za kusafisha, kutoboa na kuchana mbao
92. Kufungua mradi wa kuuza vifaa vya Umeme wa kutumia upepo
93. Biashara ya kuagiza magari
94. Kufanya biashara za Jukebox
95. Kukodisha matenki ya maji
96. Kufungua duka la kuuza Asali
97. Kutengeneza Mikokoteni/ matoroli na kuikodisha
98. Kufungua Duka la vinyago, batiki
99. Kuanzisha huduma ya AIRTEL MONEY, MPESA, TIGOPESA, EZY PESA
100. Kuanzisha sehemu ya kufanyia mazoezi (Gym).
101. Kununua na kuuza vifaa vya kupima ardhi.
102. Kufungua duka la kuuza dawa (pharmacy).
103. Kufungua Kampuni ya Ulinzi
104. Kufungua kampuni ya "Clearing and fowarding"
105. Kuchezesha vikaragosi
106. Kuuza spea za bajaji, magari na pikipiki
107. Kuuza baiskeli
108. Kuuza magodoro
109. Kuuza vyombo mbalimbali kwa ajili ya matumizi ya nyumbani mfano bakuli, sahani, vikombe,                 vijiko,
110. Kuuza marumaru (limestones)
111. Kuuza kokoto
112. Kuuza mchanga
113. Kufundisha Tuisheni
114. Biashara za bima
115. Kampuni ya kusafirisha abiria kwa njia ya anga (ndege)
116. Biashara za kitalii
117. Biashara za meli na maboti.
118. Kampuni ya kuchimba visima
119. Kufungua ofisi ya wakili/mawakili wa kujitegemea
120. Kuuza mkaa
121. Kutengeneza mashine za kutengeneza tofali
122. Kampuni ya kupima ardhi
123. Kampuni ya magazeti
124. Kuchapa (printing) magazeti
125. Kuuza magazeti
126. Kuchimba mafuta
127. Kiwanda cha kutengeneza mabati
128. Kiwanda cha kutengeneza fanicha
129. Kiwanda cha kutengeneza matairi
130. Kutengeneza vitanda vya chuma
131. Kununua nyumba katika Maghorofa (Apartments) na kuzikodisha.
132. Kukodisha makapeti
133. Kupamba maharusi na kumbi za harusi/sherehe.
134. Mashine ya kusaga na kukoboa nafaka.
135. Kazi ya ususi na kusafisha kucha.
136. Kuuza Gypsum
137. Malori ya kubeba mafuta na Mizigo
138. Duka la kuuza mboga za majani
139. Duka la kuuza maua.
140. Kampuni ya kuzoa takataka
141. Kampuni ya kuuza magari
142. Kuuza viwanja
143. Uvuvi
144. Kutengeneza na kuuza nguzo za kujengea fensi
145. Uchoraji wa mabango.
146. Duka la kuuza silaha
147. Ukumbi wa kuonesha mpira
148. Biashara ya mlm (network marketing)
149. Yadi kwa ajili ya kupaki magari
150. Mradi wa trekta za kukodisha kwa ajili ya kilimo

Monday, March 20, 2017

KUWA MAKINI KATIKA KUOSHA NYWELE ZAKO


Dawa za kulainisha nywele (relaxer) zimekuwa zinapendwa na wanawake wengi wa Afrika kwa kuwa zina uwezo wa kulainisha nywele na kumfanya apendeze na awe wa kuvutia.

Hata hivyo, wataalamu wa afya wanadai kuwa dawa hizo zinasababisha uvimbe kwenye kizazi kutokana na kemikali za dawa hizo ambazo huingia mwilini kupitia majeraha au ngozi wakati wa kupaka.

Daktari wa Manispaa ya Ilala, Laurent Chipata alifanya utafiti na kubaini kuwa dawa za nywele na vipodozi zina kemikali ambazo husababisha uzalishwaji wa vichocheo kwa kiasi kikubwa na kusababisha uvimbe kwenye kizazi uitwao fibroids au leimyoma.

“Kemikali hizi hupenya kwenye ngozi na wakati mwingine hata kwa harufu tu, husababisha kuzalishwa kwa wingi wa vichocheo aina ya estrogen ambavyo huchangia kuota kwa uvimbe wa fibroids,” anasema.

Dk Chipata anasema kukua kwa uvimbe kwenye kizazi hutokea katika kipindi ambacho mama yupo kwenye uzazi yaani kabla hajakoma hedhi.

Utafiti wa Dk Chipata ulifanywa nchini na kujumuisha wanawake wa kada tofauti tofauti wanaotumia dawa za nywele na wale wasiotumia na ukubwa wa tatizo hili ulibainika.

“Zipo kemikali tofauti tofauti zinazosababisha uvinbe kwenye kizazi, zipo za kwenye dawa za kilimo kama DDT na za kwenye mafuta ya ngozi kama vile mercury na hydroquionone,” anasema.

Dk Chipata anasema madhara yanayopatikana katika kemikali za vipodozi ni makubwa siyo tu kwenye kizazi bali nyingine husababisha saratani au kufeli kwa figo. Anatoa mfano wa kemikali ya zebaki (mercury).

“Dawa za nywele zina madhara si lazima zipenye kwenye ngozi baada ya mtu kupata jeraha la kuungua bali zinaweza kupenya zenyewe kwenye ngozi kutokana na mfumo wa ngozi,” anasema.

Anashauri kuwa ni vyema watu wakasoma kipodozi kimetengenezwa kwa nini kabla ya kukitumia na kuongeza kuwa ni salama zaidi kubaki na ngozi au nywele halisi badala ya kujibadilisha.

Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) imekataza vipodozi vyenye kemikali kama biothionol, hexachlorophene, mercury, vinyl chloride, zirconium na bidhaa zenye aerosol, chloroquionone, steroids, methylene na chloroform.

Utafiti mwingine uliofanywa mwaka 2012 na Dk Lauren Wise na wenzake nchini Marekani na kuchapishwa kwenye jarida la afya la nchini Marekani ulibaini kuwa vipodozi vingi vina kemikali zenye vichocheo vya estrogen ambavyo kwa kawaida huchochea kasi ya kuota kwa uvimbe kwenye kizazi cha mwanamke na wakati mwingine kwenye mji wa mimba. Kitaalamu uvimbe au vivimbe hivi hujulikana kama fibroids au myoma.

Dk Wise anasema aliwafanyia uchunguzi wanawake wanaotumia dawa za kulainisha nywele na kuangali umri walioanza kutumia dawa hizo, mara ngapi, waliungua kiasi gani na walikaa na dawa hizo kichwani kwa kipindi gani.

Aliwafuatilia wanawake 23,580 wanaotumia dawa za kulainisha nywele na baada ya kipindi fulani walipimwa. Kati yao, 7146 waligundulika kuwa na uvimbe kwenye kizazi baada ya kupimwa kwa mionzi na wengine kufanyiwa upasuaji.

Kwa nini relaxer ni hatari kwa wanawake?
Dk Wise anasema mchanganyiko ulio kenye dawa za nywele hasa zilizoandikwa “Lye Relaxer” ni sodium hydroxide wakati makopo ya dawa yaliyoandikwa “No Lye Relaxer” yana calcium hydroxide na guanidine carbonate.

Bidhaa za kulainishwa nywele zilizoandikwa ‘no lye relaxer’ zinadaiwa kusababisha majeraha kwa kiasi kidogo ukilinganisha na zile zilizoandikwa “Lye Relaxer”.

FAIDA YA TANGAWIZ KIAFYA

Asante kwa kuendelea kutembelea Mbinuzamafanikio.blogspot.com, kwani tunaamini ya kwamba unaimarika sana kifkra kupitia makala hizi. 

ambo la msingi katika makala ambazo unazisoma kupitia ukurasa huu unatakiwa kuchukua hatua, hii itakuwa njia bora zaidi la kuweza kutimiza lile kusudio lako.

Tukiachana na hayo naomba nikukaribishe katika Makala haya, kwani siku ya leo tutazungumzia umuhimu wa tangawizi katika kutibu magonjwa mbalimbali. Kwani naamini kila mmoja wetu anaifahamu vyema tangawizi.

Zifuatazo ndizo faida za tangawizi.

1. Tangawizi hutibu matatizo ya koo pamoja na kukauka kwa sauti.

Unachotakiwa kufanya ni:
Tafuna vipande vidogo vya Tangawizi.

2. Tangawizi huzuia kichefuchefu na kutapika.

Unachotakiwa kufanya:
Kunywa mchanganyiko wa Juice ya Tangawizi.

3.Husaidia kutibu maumivu makali ya tumbo.

Unachotakiwa kufanya ni :
Changanya kijiko kimoja cha au viwili vya Tangawizi iliyosagwa na kijiko kimoja au viwili vya mafuta ya Kastoli. Kunywa kijiko kimoja mara mbili kwa siku.

4.Tangawizi husaidia kwa kiwango kikubwa matitizo ya kuuma kwa meno pia husaidia kutibu maumivu ya kichwa.

Unachotakiwa kufanya ni:
Chukua Tangawizi ya Unga koroga na maji kidogo iwe nzito kama tope. Jipake na uchue kwenye paji lako la uso kabla ya kulala. Kwa Jino jipake na uchuwe kwenye Shavu.

6. Hutibu mafua makali na kikohozi, osha na kisha

Unachotakiwa kufanya ni :
Twanga tangawizi na uichemshe katika maji kwa muda mrefu.
Unaweza kuweka majani ya chai au maziwa na kisha kunywa taratibu ikiwa ya moto. Fanya hivyo kwa siku mbili na mafua yatapona kabisa.

Lakini kabla akaweka nukta matumizi mengine ya  tangawizi ni kurekebisha matumizi ya kina mama katika zile siku ngumu. Mathalani, iwapo tarehe zinabadilika mara kwa mara unaweza kutumia kurekebisha mwenendo wa siku hizo muhimu.

FAIDA YA TANGAWIZ KIAFYA

Asante kwa kuendelea kutembelea Mbinuzamafanikio.blogspot.com, kwani tunaamini ya kwamba unaimarika sana kifkra kupitia makala hizi. 

ambo la msingi katika makala ambazo unazisoma kupitia ukurasa huu unatakiwa kuchukua hatua, hii itakuwa njia bora zaidi la kuweza kutimiza lile kusudio lako.

Tukiachana na hayo naomba nikukaribishe katika Makala haya, kwani siku ya leo tutazungumzia umuhimu wa tangawizi katika kutibu magonjwa mbalimbali. Kwani naamini kila mmoja wetu anaifahamu vyema tangawizi.

Zifuatazo ndizo faida za tangawizi.

1. Tangawizi hutibu matatizo ya koo pamoja na kukauka kwa sauti.

Unachotakiwa kufanya ni:
Tafuna vipande vidogo vya Tangawizi.

2. Tangawizi huzuia kichefuchefu na kutapika.

Unachotakiwa kufanya:
Kunywa mchanganyiko wa Juice ya Tangawizi.

3.Husaidia kutibu maumivu makali ya tumbo.

Unachotakiwa kufanya ni :
Changanya kijiko kimoja cha au viwili vya Tangawizi iliyosagwa na kijiko kimoja au viwili vya mafuta ya Kastoli. Kunywa kijiko kimoja mara mbili kwa siku.

4.Tangawizi husaidia kwa kiwango kikubwa matitizo ya kuuma kwa meno pia husaidia kutibu maumivu ya kichwa.

Unachotakiwa kufanya ni:
Chukua Tangawizi ya Unga koroga na maji kidogo iwe nzito kama tope. Jipake na uchue kwenye paji lako la uso kabla ya kulala. Kwa Jino jipake na uchuwe kwenye Shavu.

6. Hutibu mafua makali na kikohozi, osha na kisha

Unachotakiwa kufanya ni :
Twanga tangawizi na uichemshe katika maji kwa muda mrefu.
Unaweza kuweka majani ya chai au maziwa na kisha kunywa taratibu ikiwa ya moto. Fanya hivyo kwa siku mbili na mafua yatapona kabisa.

Lakini kabla akaweka nukta matumizi mengine ya  tangawizi ni kurekebisha matumizi ya kina mama katika zile siku ngumu. Mathalani, iwapo tarehe zinabadilika mara kwa mara unaweza kutumia kurekebisha mwenendo wa siku hizo muhimu.

Saturday, March 18, 2017

Namna ya kupata wateja

Katika ushindani wa kibiashara uliopo na mabadiliko ya kiuchumi na kiteknolojia, kupata wateja kumekuwa kugumu sana. Hivyo ili ufanikiwe kweli katika biashara inabidi sio tuu uwe na bidhaa nzuri lakini pia ujue namna bora ya kutafuta wateja.

Hata kama una duka la nguo tuu dogo au saluni waweza kuwa umeathirika na namna ambavyo ushindani wa biashara ulivyo. Hivyo katika makala hii utajifunza mbinu ya kisasa kabisa ya kupata wateja wa biashara yako.

Kabla ya kujifunza  mbinu ya jinsi ya kupata wateja unahitaji kujua kwanza kwanini ni ngumu kupata wateja.

Hali ngumu ya kiuchumi : Kuna namna mbili ambapo hali ya kiuchumi inaweza athiri kupatikana kwa wateja. Kwanza kuwafanya wasiwe na uwezo wa kulipia bidhaa yako , na pili kuwafanya wajifikirie sana kuhusu kununua bidhaa zako. Katika yote haya hali ngumu ya kiuchumi inajenga ukinzani wa wewe kujenga ushawishi kwa wateja wako kununua bidhaazako.

Mabadiliko ya teknolojia: Teknolojia inafanya watu wengi zaidi waweze kuwafikia wateja wako ambapo hapo kabla haikua rahisi. Enzi hizo ilikua utengeneze vipeperushi au uwe na hela za kutosha kutangaza redio, kwa tv na kwenye mabango. Ila sasa watu kupitia Facebook, WhatsApp, na Instagram wanaweza kuwafikia watu wengi kwa urahisi. Hata yule mtengeneza keki mtaani kwenu nae yupo Instagram akitangaza keki na mikate yake. Bwana Mangi nae yupo kwa Facebook akitafuta wateja wa kibanda chake cha kuuza vocha za simu na MPESA.

Njia ya kisasa ya kisasa ya kuwapata wateja:

Tumefika wakati ambapo wateja wengi wana taarifa nyingi kuhusu wapi na kwa bei gani bidhaa zinapatikana. Hivyo wewe kuwa tuu na bidhaa fulani au kwa bei fulani hakutoshi kuwa njia ya kuwafikia.

Pia kwakua kuna watangazaji wengi wa bidhaa inakupasa wewe kuwa na namna ya kipekee ya kuwafikia wateja wako bila kuwa kero kwa wateja kama walivyo watu wengine wengi ambao ni wazi kabisa kwa “makelele” yao ya matangazo wanaonekana wazi wanachotaka wao ni kuuza tuu hizo bidhaa waishie zao. Ni ukweli wa kitaalamu katika marketing kuwa watu wengi  hawapendi kujisikia kuwa fulani anawauzia bidhaa. Hata hivyo hivyo haimaanishi kuwa watu hawapendi kununua. Watu hupenda kununua ila hawapendi ile hali ya kuwekwa “kati” na mtu anayejaribu kuwauzia kitu.

Ukichanganya na ukweli huo kuwa watu hawapendi kujisikia wakiuziwa bidhaa, halafu hali ngumu ya uchumi na mabadiliko ya teknolojia yanafanya kuwepo na “makelele” ya wafanyabiashara wengi,  basi wewe unahitaji mbinu ya ziada.

Hivyo basi mbinu ya kisasa ninayozungumzia hapa ni kutengeneza ushirika na wateja kama jamii ambayo itakuamini na kukuona una kitu zaidi ya kutaka tuu kuwauzia bidhaa zako. Kwa mbinu hii unajenga uhusiano na kufikia hisia za wateja wako, unatambua matatizo yao , unakua kweli mshirika wao katika yale ambayo unaona wao wanaweza kunufaika kupitia bidhaa zako hapo baadae.

Kwa mfano kama wewe ni muuza nguo, badala ya kila wakati kuwatangazia tuu mzigo mpya ulio nao, tambua kwanini hawa watu wanunue nguo mpya. Zungumza nao kuhusu hayo mambo. Mfano iwe ni swala la kujisitiri, au unadhani wananunua sana kwa ajili ya kujionyesha kuwa wanaenda na wakati na ni watu wa mitindo, basi waonyeshe unalielewa hilo kwa kutumia mitandao ya kijamii ukipost vitu vinavyoendana na hayo mambo ya mitindo na kuenda na wakati.

Jiweke katika nafasi zao, na uwahudumie vema kihisia kwanza , ukishawaonyesha kuwa wewe unaweza na unajua nini wanataka , hapo ni rahisi kuwaambia kuhusu bidhaa zako ambazo zitawafikisha katika malengo hayo wanayodhamiria.

Kwa mbinu hii unaondoa upinzani wa wateja kutaka kukusikiliza , na unafanya rahisi kwa wao kufanya maamuzi ya kununua bidhaa zako kwakua hawaoni kama unawauzia bidhaa, bali wanaona ni muendelezo wa ukaribu wako na utayari wako wa kuwaona wakijisikia vizuri na kufikia malengo yao.

Katika kutengeneza huo ukaribu wako na wao kupitia machapisho, videos, na picha mbalimbali wenyewe wateja wajisikia utayari wa kukutafuta. 

Namna ya kuandaa mpango biashara (B ussiness plan)

Watu wengi kwa karne ya sasa huishi kwa malengo ya kuwa watu fulani au watu wanaomiliki vitu fulani,yote hayo yanaweza kufanikiwa endapo mtu/watu hao wapo tayari kufanya kazi kwa juhudi na maarifa kwa kutumia viungo na akili zetu ambazo tumepewa bure na Mwenyezi Mungu bila malipo yoyote.

Kutokana na changamoto tofauti tofauti katika soko la ajira ikiwa sambamba na ufinyu wa upatikanaji wa ajira zenyewe lakini pia maslahi duni, manyanyaso na mateso yanayopatikana sehemu sehemu za kazi, watu wengi kwa sasa wanaona ni bora wafikirie kuitwa WAAJIRI  na si WAAJIRIWA tena.

Pamoja na matamanio hayo, watu wengi wamekutana na changamoto kubwa katika kuanzisha au kuendeleza biashara hizo. Naomba nieleweke wazi biashara si lazima kununua na kuuza,yaweza kuwa ya kuzalisha na kuuza pia, hapa nazungumzia kujenga na kupangisha, kulima na kuuza, utoaji wa huduma uliyosomea n.k.

Yote hayo na mengine mengi utafanikiwa endapo tu utakuwa na MPANGO BIASHARA katika aina yoyote ya biashara unayofanya au unayotaka kufanya. Mtandao huu kwa kutambua juhudi kubwa za wasomaji wake kutaka kujikomboa kiuchumi leo tunakuletea jinsi ya kuandaa MPANGO BIASHARA (BUSINESS PLAN) ILI UFANIKIWE. Huu utakuwa ni mfululizo wa makala mbali mbali za UCHUMI NA BIASHARA PAMOJA NA FURSA MBALI MBALI UNAZO WEZA KUZITUMIA HAPO HAPO UNAPOISHI.

UTANGULIZI

Mpango biashara Biashara ni nyaraka muhimu sana kwa biashara yako kwakuwa inakupa picha ya matarajio ya namna biashara itakavyokuwa. Ukifanya mchanganuo huo kwa ufasaha kama inavyoelekezwa utaweza kutambua kama kweli biashara unayotaka kuifanya itakulipa au la. Pia utaweza kutambua matatizo na changamoto kabla haujaanza biashara.

Mpango Biashara kwa kiwango flani unahitaji utafiti ili kuweza kuandika vema mambo yanayoendana na biashara yako. Mfano unahitaji kufanya utafiti wa soko ili kujua kwa biashara yako ni akina nani hasa watakuwa wateja wako, na kwanini watakuja kununua bidhaa kwako. Pia unahitaji kufanya utafiti wa gharama utakazotumia kuendesha biashara. Pia gharama za ununuzi wa samani pale utapoendeshea biashara yako,kama Meza, Kiti n.k

Mpango Biashara unakuhitaji ujue picha kubwa ya mazingira ya biashara yako pindi utakapoianzisha. Mfano masuala ya Kodi, Masuala ya Kisheria kama vile Sheria za Ajira, Vibali, Uendeshaji wa Biashara n.k.

Na mwisho kama unataka kuandika Mpango Biashara ili ukaombe mkopo, basi fikiria kwa umakini namna ambavyo utakuja kuulipa mkopo husika. Umejipangaje katika usimamizi makini wa biashara yako.

Ufuatao ni mtiririko wa mchanganuo wa biashara.

Jalada la nje: Linahusisha jina la biashara, muda wa mpango (mfano. 2016 – 2020), anuani ya biashara, toleo, jina la aliyeandaa, mwaka pamoja na kuonyesha mchanganuo unaelekezwa kwa nani.

Dibaji: Sehemu hii huandikwa muhtasari wa mambo mbalimbali yaliyoanishwa katika mchanganuo mathalani, aina ya biashara, bidhaa au huduma zinazotolewa kwa ufupi, mpango wa mauzo, mpango wa ukuaji kwa mwaka, soko lengwa, mtaji unaohitajika, namna mwekezaji au mdau anavyoweza kunufaika iwapo akiwekeza au benki ikikupatia mkopo namna gani utalipa.

Maelezo ya biashara: Dira/ndoto, madhumuni, historia fupi ya biashara, bidhaa au huduma inayotolewa kwa mapana, uchanganuzi wa hali ya tasnia kwa sasa na siku zijazo, uchanganuzi wa hali ya biashara kwa kuainisha upungufu na nguvu ndani ya biashara, fursa na vihatarishi katika mazingira yanayoizunguka biashara.

Masoko: inazungumzia hali ya soko katika tasnia ya biashara husika, soko unalopanga kuuzia bidhaa au huduma, unaweza kuchukua nafasi gani katika soko hilo kwa asilimia.

Mbinu unazotumia kufikisha bidhaa au huduma kwenye soko, mpango wa mauzo kwa mwezi, kwa mwaka hadi muda wa mpango uliojiwekea mathalani miaka 3 hadi miaka 5, mpango wa bei, hali ya ushindani, mbinu za kuendana na ushindani katika soko, namna ya kutangaza biashara, na unapaswa kuangalia ni jinsi gani utaweka kipaumbele katika kutangaza bidhaa kama una zaidi ya bidhaa moja.

Menejimenti na Utawala: Mfumo wa biashara kama ni ya mtu mmoja, ubia au kampuni, chora chati ya mtiririko wa madaraka, wasifu wa maofisa wa ngazi za juu mathalani Mkurugenzi Mtendaji na wakurugenzi wengine, idadi ya wafanyakazi kwa sasa, mpango wa ukuaji au kuongezeka kwa wafanyakazi, mfumo wa umiliki kama ni kampuni-weka mchanganuo wa hisa za kila mmliki, kama ni ubia elezea mchango wa kila mmoja na namna ya kugawana maslahi, toa mchanganuo kwa wataalam mbalimbali unaowatumia katika biashara mathalani mshauri wa biashara, mwanasheria, wasafirishaji na wakaguzi.

Masuala ya Fedha: Weka makisio ya mizania, mapato na matumizi na mtiririko wa fedha kwa muda wa mpango tangu sasa.

Maelezo ya dhana ya kifedha iliyotumika kupanga makisio, muundo wa mtaji (ainisha kiasi cha mtaji binafsi, msaada, mikopo, na njia nyinginezo kama zipo).

Mwisho ni mpango wa kupata fedha kama zinatoka kwa wawekezaji au benki- kiasi gani unahitaji kwa muda gani na namna gani utalipa kwa faida gani.

Mchanganuo wa vihatarishi vya biashara: Ainisha vihatarishi vya biashara yako, fursa za kibiashara zinazoendena na vihatarishi hivyo, mchanganuo wa itakuwaje endapo mipango uliyojiwekea haitatekelezeka, mchanganuo vihisishi, kwa mfano namna gani bei ikipanda au kushuka inaweza kubadilisha mwelekeo wa biashara yako.

Ratiba ya uzalishaji bidhaa au utoaji huduma:  Mara nyingi  ratiba ya uzalishaji inafanywa kwa programu za kinakilishi.

Viambatanisho: Viambatanisho mbalimbali huwekwa kulingana na mtumiaji wa mchangunuo huo mathalani wasifu binafsi wa maofisa wa ngazi za juu, nakala ya vyeti vya usajili, TIN, leseni na vibali vya biashara.

KWA UFUPI VITU  VYA KUZINGATIA KATIKA KUANDAA MPANGO BIASHARA

Muhtasari wa biashara yakoHistoria na maelezo ya biashara yakoMaelezo ya bidhaa au huduma ya biashara yakoMchanganuo wa masokoUkubwa wa sokoMgawanyo wa sokoAina ya soko/masokoMchanganuo wa ushindaniWatoa huduma au wauza bidhaa kama yakoUdhaifu waoUwezo waoMkakati wa utekelezajiUongozi na usimamizi wa kaziUchambuzi wa madhaifu, nguvu, fursa na hatari zinazokabili biashara yakoMkakati wa UzalishajiMkakati wa kuuzaMpango wa fedhaUchambuzi wa mahitaji ya mtajiWapi utatoa mtajiMatumizi ya mtajiMakisio ya MauzoUchambuzi wa kurudisha gharama (break even analysis)Makisio ya faida au hasaraMakisio ya mzunguko wa fedha katika biashara yako (cashflow)Makisio ya oanisho la mali na madeni ya biashara yako (balance sheet)Ulinganifu wa sehemu mbalimbali za biashara (business ratios)LeseniCheti cha ulipaji kodiCheti cha usajiliTaarifa mbalimbali za biashara yako ambazo hazikupata nafasi ndani ya mchanganuo huu.

 

NAMNA YA KUJUA KUSUDI LAKO ULILOPEWA N.A. MUNGU

Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la BWANA ndilo litakalosimama. (MIT. 19:21 SUV).

Tafsiri ya Bibilia ya Habari Njema inasema:

Kichwani mwa mtu mna mipango mingi, lakini anachokusudia Mwenyezi-Mungu ndicho kitakachofanyika. (Methali 19:21 BHN).

Tafsiri ya Neno inasema:

Kuna mipango mingi ndani ya moyo wa mtu, lakini kusudi la BWANA ndilo litakalosimama.

Tukijumuisha yale yasemwayo katika tafsiri zote hizi tatu tunaweza kutoa muhtasari kwa kusema,

Japokuwa tunapanga mipango mingi ni ile iliyo sawa na kusudi la Bwana kwa ajili yetu ndiyo itakayo simama.

Sasa kama ni kusudi la Bwana ndilo litakalo simama, kwanini tupoteze muda kupanga mipango ambayo hatuna uhakika ni kusudi la Bwana au la kwa ajili yetu? Kwanini kusiwe na namna ya kujua kusudi la Mungu kwa ajili yetu ili tunapopanga mipango yetu tuipange kwa kuzingatia kusudi la Bwana kwa ajili yetu?

Tena maandiko yanaendelea kusema sehemu nyingine:

Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo. (EFE. 2:10 SUV).

Kumbe Mungu alipotuumba, alituumba ili tutende matendo mema fualni maalum ambayo yalishaandaliwa ili tuenende nayo. Sasa kwanini nisijue yale ambayo niliumbwa niyafanye alafu niyafanye?

Mungu anatuambia kwenye kitabu cha Yeremia:

Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho. (YER. 29:11 SUV).

Kwa mujibu wa hili andiko yapo mawazo ambayo Mungu anatuwazia sisi. Ni mawazo ya mema na siyo ya mabaya, kutupa mwisho uliyojaa matumaini.

Tafsiri ya Bibilia ya Habari Njema inasema:

Maana, mimi Mwenyezi-Mungu ninajua mambo niliyowapangia. Nimewapangieni mema na si mabaya, ili mpate kuwa na tumaini la baadaye. (Yeremia 29:11 BHN).

Kwa hiyo ipo mipango ambayo. Mungu ametupangia. Ametupangia mema na si mabaya ili tuwe na tumaini la baadaye.

Sasa kama Mungu anayo mawazo mazuri kwa ajili yetu, na Mungu anayo mipango mizuri kwa ajili yetu, kwanini tusitafute kujua hayo mawazo na hiyo mipango ili nasi tuwaze na kupanga sawa na hiyo? Maana Yeye anajua kwanini alituumba na Yeye anajua alituumbia uwezo wa kufanya nini ndani yetu. Kwanini tusitafute kuyajua mawazo ya Mungu kwa ajili yetu na mipango hiyo aliyo nayo kwa ajili yetu ili tusiishi maisha yetu tukipoteza tu muda na mipango ambayo sio ya Mungu kwa ajili yetu ambayo haiwezi kufanikiwa hata hivyo?

Tafsiri ya Neno ya andiko hili la Yeremia inasema:

Kwa maana ninajua mipango niliyo nayo kwa ajili yenu,’’ asema BWANA. “Ni mipango ya kuwafanikisha na wala si ya kuwadhuru, ni mipango ya kuwapa tumaini katika siku zijazo.

Mipango ya Mungu kwa ajili yetu itatufanikisha. Mafanikio yetu katika maisha haya yanategemea sisi kulifahamu kusudi la Mungu kwa ajili ya maisha yetu na kutembea katika hilo.

Napenda maneno ninayoyasoma katika kipande cha mstari kwenye kitabu cha Waefeso:

na ndani yake sisi nasi tulifanywa urithi, huku tukichaguliwa tangu awali sawasawa na kusudi lake yeye, ambaye hufanya mambo yote kwa shauri la mapenzi yake. (EFE. 1:11 SUV).

Mungu hufanya mambo yote kwa kushauriana na mapenzi Yake kwa ajili yako. Kama hilo analotakwa alifanye litasaidia katika kudhibitisha mapenzi Yake katika maisha yako atalifanya. Kama analotakwa alifanye litavuruga mapenzi ya Mungu katika maisha yako, hakika hatalifanya.

Najuaje sasa mapenzi ya Mungu kwa ajili yangu? Naujuaje huo mpango wa Mungu kwa ajili yangu?

Kwanza kabisa badilisha kufikiri kwako. Anza kufikiri kwa namna ambayo kutaweka madai kwenye upeo wa kufikiri kwako juu ya kuujua mpango wa Mungu kwa ajili ya maisha yako.

Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu. (RUM. 12:2 SUV).

Ukifanya upya nia yako utajua mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yaliyo kubalika na yaliyo kamili kwa ajili ya maisha yako.

Akili yako lazima igeuzwe. Akili yako lazima ibadilishwe. Kinachoweza kubadilisha akili yako kwa kiwango hicho ni kusoma kwako kwingi. Usomaji wako kwa wingi kutakugeuza akili yako na kupanga kufikiri kwa akili yako sawa na kusudi la Mungu na mapenzi ya Mungu kwa ajili yako.

Alipokuwa akijitetea hivi, Festo akasema kwa sauti kuu, Paulo, una wazimu, kusoma kwako kwingi kumekugeuza akili. (MDO 26:24 SUV).

Sasa ni nini hicho natakiwa kukisoma kwa wingi ili akili zangu zigeuzwe, zifanywe upya ili nipate kuyajua mapenzi ya Mungu kwa ajili yangu alafu nitembee katika hayo?

Macho yako yaliniona kabla sijakamilika; Chuoni mwako ziliandikwa zote pia, Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado. Mungu, fikira zako zina thamani nyingi kwangu; Jinsi ilivyo kubwa jumla yake! Kama ningezihesabu ni nyingi kuliko mchanga; Niamkapo nikali pamoja nawe. (ZAB. 139:16-18 SUV).

Siku zangu na zako zilizoamriwa na Mungu zimeandikwa chuoni mwa Mungu au katika neno la Mungu. Tunapokuwa wasomaji wazuri wa neno la Mungu, siku zetu zilizoamriwa na fikra au mawazo au mipango ya Mungu kwa ajili yetu inafunuliwa kwetu.

Kumbuka hili:

Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu. (ZAB. 119:105 SUV).

Neno la Mungu ni taa ya miguu yetu ikimaanisha itatusaida kuona tulipokanyaga, tulipo sasa hivi na ni mwanga wa njia yetu maana yake litatuonyesha tunapopaswa kwenda.

Nimalize kwa andiko hili:

Ndipo niliposema, Tazama nimekuja, (Katika gombo la chuo nimeandikiwa,) Kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu; Naam, sheria yako imo moyoni mwangu. (ZAB. 40:7, 8 SUV).

Ukishajua yale yaliyoandikwa kukuhusu kwenye gombo la chuo kwa ajili yako ni rahisi kuyafanya mapenzi ya Mungu uliyozaliwa kuyatumikia. 

Jenga ukaribu na neno la Mungu. Lisome kwa wingi neno la Mungu. Litakufungua kuwaza ikupasavyo kwa habari ya mpango wa Mungu kwa ajili yako.

HISTORIA YA MWALIMU JULIUS K.NYERERE

HISTORIA FUPI YA MWALIMU NYERERE
MPAKA MAUTI YALIPOMFIKA

Tarehe ya kuzaliwa 13 Aprili 1922
Mahali pa kuzaliwa Butiama
Tarehe ya kifo 14 Oktoba 1999
Rais wa Tanzania
Alingia ofisini 1964
Aliondoka ofisini 1985
Alitanguliwa na (alikuwa rais wa kwanza)
Alifuatwa na Ali Hassan Mwinyi
Dini Mkristo Mkatoliki
Elimu yake Chuo Kikuu cha Edinburgh - Uskoti Digrii
anazoshika M.A. ya historia na uchumi
Kazi mwalimu, mwanasiasa Mengine Nyerere alikuwa
mwenyekiti wa chama cha TANU na baadaye wa CCM.
Mara nyingi aliitwa "Mwalimu Nyerere".
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alikuwa rais wa
kwanza wa Tanzania. Alizaliwa Butiama, mkoani Mara
pembezoni mwa Ziwa Nyanza tarehe 13 Aprili, 1922.
Alifariki dunia 14 Oktoba, 1999. Aliiongoza Tanzania toka
mwaka 1961 hadi mwaka 1985.
Yeye ni mwasisi wa itikadi ya ujamaa na kujitegemea.
Kabla ya kuingia kwenye siasa alikuwa ni mwalimu. Kazi
hii ndiyo ilimpatia jina ambalo lilimkaa maisha yake yote la
"Mwalimu." Mwalimu Nyerere ni kati ya viongozi wachache
wa Afrika ambao wameacha madaraka kwa hiyari baada
ya kutawala kwa muda mrefu. Alipostaafu urais mwaka
1985 alirudi kijijini kwake Butiama ambako aliendesha
shughuli za kilimo. Aliendelea kuwa na athari kubwa
katika siasa ya Tanzania hadi kifo chake.
Maisha Ya Mwalimu
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alizaliwa mwaka 1922
( katika kijiji cha Butiama, wilaya ya Musoma, mkoa wa
Mara, Tanzania (wakati ule: Tanganyika). Alikuwa
mojawapo kati watoto 26 wa Nyerere Burito, chifu wa
kabila la Wazanaki. Alipokuwa mtoto Nyerere alichunga
mifugo ya babake; katika umri wa miaka 12 aliingia shule
akitembea kilomita 30 hadi Musoma. Baada ya kumaliza
shule ya msingi aliendelea kusoma shule ya wamisionari
Wakatoliki huko Tabora. Katika umri wa miaka 20
alibatizwa akawa mkristo Mkatoliki hadi mwisho wa
maisha yake.
Mapadre wakaona akili yake wakamsaidia kusoma ualimu
huko Makerere, Kampala, Uganda kuanzia 1943 - 1945.
Makerere akaanzisha tawi la Umoja wa wanafunzi
Watanganyika pia amejihusisha na tawi la Tanganyika
African Association (TAA). Baada ya kumaliza masomo ya
ualimu alirudi Tabora akifundisha shule ya St.Mary´s.
Mwaka 1949 alipata skolashipu ya kwenda kusoma
kwenye Chuo Kikuu cha Edinburgh huko Uskoti /Uingereza
akasoma M.A. ya historia na uchumi(alikuwa mtanzania
wa kwanza kusoma katika chuo kikuu cha Uingereza na
mtanzania wa pili kupata shahada ya elimu ya juu nje ya
Tanzania).
Aliporejea Tanganyika kutoka masomoni, Nyerere
alifundisha Historia, Kingereza na Kiswahili katika shule ya
St. Francis iliyo karibu na Dar es Salaam. Mwaka 1953
alichaguliwa kuwa raisi wa chama cha Tanganyika African
Association (TAA), chama ambacho alikisaidia kukijenga
alipokuwa mwanafunzi katika chuo kikuu cha Makerere.
Mwaka 1954 alikibadilisha chama cha TAA kwenda katika
chama cha Tanganyika African National Union (TANU)
ambacho kilikuwa cha kisiasa zaidi kuliko TAA. Ndani ya
mwaka mmoja chama cha TANU kilikuwa tayari chama cha
siasa kinachoongoza Tanganyika.
Uwezo wa mwl. Nyerere uliwashitua uongozi wa kikoloni
na kumlazimisha Nyerere kuchagua kati ya siasa na kazi
ya ualimu. Nyerere alisikika akisema kuwa alikuwa
mwalimu kwa kuchagua na mwanasiasa kwa bahati
mbaya. Alijiuzuru ualimu na kuzunguka nchini Tanganyika
kuzungumza na watu wa kawaida na machifu ili kuleta
muungano katika mapigano ya uhuru. Pia alizungumza
kwa niaba ya TANU katika Trusteeship council na Fourth
committee ya Umoja wa Mataifa (UN) huko New York.
Uwezo wake wa kimaongezi na kuunganisha watu
ulimwezesha kufanikisha Tanganyika kupata uhuru bila
umwagaji wa damu. Ushirikiano mzuri aliouonyesha
aliyekuwa gavana wa wakati huo bwana Richard Turnbull
ulisaidia pia kuharakisha upatikanaji wa uhuru. Nyerere
aliingia katika bunge la kikoloni mwaka 1958 na
kuchaguliwa kuwa waziri mkuu mwaka 1960. Mwaka 1961
Tanganyika ilipata uhuru wake na tarehe 9/12/1961
Nyerere alichaguliwa kuwa waziri mkuu wa Tanganyika
huru na mwaka mmoja baadae Nyerere alikuwa raisi wa
kwanza wa jamhuri ya Tanganyika. Nyerere alikuwa kiungo
muhimu katika muungano wa Tanganyika na Zanzibar
kutengeneza Tanzania baada ya mapinduzi ya Zanzibar
mwaka 1964 yaliyomtoa madarakani sultani wa Zanzibar
Jamshid bin Abdullah.
Sifa zake
Bado anakumbukwa na watanzania hasa wa hali ya chini
kutokana na sera zake za kujali utu na ubinadamu.Pia
ataendelea kukumbukwa na waafrika kote barani hasa kwa
mchango wake mkubwa wakati wa harakati za kupigania
uhuru katika nchi mbali mbali barani Afrika.
Ni mmoja wa viongozi wachache wanaokumbukwa kwa
kutojilimbikizia mali pamoja na kutawala kwa miaka zaidi
ya 24.
Mwishoni mwa maisha yake Nyerere aliishi kama mkulima
wa kawaida kijijini kwake Butiama. Alipatwa na kansa ya
damu (leukemia) na kufariki Uingereza wakati wa kutibiwa
katika mji wa London tarehe 14 Oktoba, 1999. Alizikwa
mahali pa kuzaliwa kwake, kijiji cha Butiama.
Machapisho ya mwl.Julius K. Nyerere.
• Freedom and Socialism.Mkusanyiko wa maandiko na
hotuba, 1965-1967 (1968)
• Freedom & Development, Uhuru Na Maendeleo (1974)
• Ujamaa - Essays on Socialism' (1977)
• Crusade for Liberation (1979)

TIBA TOSHA YA KISUKARI KWA KUTUMIA CHAKULA N.A. MAZOEZI

Kwa mgonjwa wa kisukari anashauriwa kuweza kufanya yafuatayo ili kuweza kupunguza kiwango cha sukari katika mwili wake. Kwani inasadikika ya kwamba kwa mgonjwa wa kisukari anatakiwa kuwa na kiwango cha kati cha sukari katika damu, kwani pindi sukari ikipungua sana (Hypoglycemia) au sukari ikizidi (Hyperglycemia) huwa ina athari kubwa kiafya.

Hivyo kwa kuzingatia ushauri mbalimbali wa wataalamu wa afya wanasema ya kwamba, ili kuweza kuweza kufanya kiwango cha sukari kuwa katika hali ya kawaida unashauriwa kufanya yafuatayo:

1. Kula chakula cha wanga kwa wingi.
Mgonjwa wa kisukari hana masharti ya ajabu kuhusu chakula anachotakiwa kula, kimsingi anaweza kula chakula chochote anachopenda. Kuna mambo matatu ambayo yanabidi kuangaliwa katika kuweka kiwango cha sukari cha mgonjwa kwenye kiwango kinachofaa. Mambo hayo ni:

-Ni chakula gani-Chakula hicho kinaliwa kwa kiasi gani-Chakula hicho kinaliwa muda gani

Watalaamu wa afya na mambo ya chakula wanabainisha kwamba chakula kinachotakiwa kuliwa kwa wingi zaidi ni chakula chenye wanga (carbohydrates), kikifuatiwa na mboga na matunda, kisha chakula chenye protini na mwisho ni chakula chenye mafuta (fats).

Tunapozungumzia chakula Chenye Wanga hapa tuna maana chakula ambacho kinapatikana zaidi kati mboga za majani,  nafaka,  matunda pamoja na maziwa ya mgando. Wataalamu wanasisitiza kula chakula hiki cha wanga kwani aina hiyo ya vyakula husaidia katika kuzalisha glucose ambazo husaidia kuweza kujenga nguvu za mwili na kuupa nguvu mwili.

Lakini kama hiyo haitoshi imeshauriwa ya kwamba pindi mtu akila kiasi kile kile cha chakula chenye wanga na muda ule ule kila siku, anakuwa na nafasi kubwa sana ya kudhibiti kiwango chake cha sukari katika mwili wake.

Lakini vilevile tunashauriwa na watalamu wa afya ya kwamba Kuchanganya aina tofauti tofauti za nafaka, matunda na mboga kumeonyesha kusaidia  zinasidia kupunguza kiwango cha sukari mwilini.

Hivyo ili kuweza kupunguza kiwango cha sukari hakikisha unatumia chakula ambacho nafaka zake ni zile ambazo hazikukobolewa. Na pia matunda hakikisha inayotumia yakiwa na maganda yake. Kwani kwa baadhi ya matunda vitamini yake ipo katika matunda.

Kwa leo naomba tuishie hapo usikose kusoma mwendelezo wa makala haya siku ya kesho, tutazungumzia umuhimu wa mazoezi kwa mgonjwa wa kisukari .

Maana ya herufi M kiganjani


Watu wengi wanasema, mistari katika viganja vya kila binadamu vimebeba mambo mengi na maana nyingi kuhusu tabia yako na hatima yako kwa ujumla.

Pia inasemekana watu wenye herufi 'M' katika viganja vyao,ni watu wa aina muhimu sana.Inasemekana watu hawa wana sifa za ajabu.Wana ushirikiano mzuri na wafanyakazi katika aina yeyote ile ya biashara.

Kama una mpenzi mwenye alama 'M' katika kiganja chake,basi yakupasa kujua yupo makini katika uhusiano wenu.Hakuna utani,hakuna uongo na hakuna udanganyifu.

Watu wenye herufi 'M' katika viganja vyao, wana uwezo mkubwa wa kufanya mabadiliko katika maisha yao na daima utumia vizuri fursa wanazozipata katika maisha yao.

Imekuwa ikijulikana kwa watu wa zamani, kwamba manabii wote walikuwa na alama hii katika mikono yao.

Angalia mkoni wako na endapo ukijikuta una alama ya 'M' basi tambua kwamba wewe ni mtu maalamu.

Faida za mlonge

Mlonge, mlongo, mronge, mrongo, mkimbo au mzunze (Moringa oleifera) ni mti wa jenasi pekee, Moringa, ya familia Moringaceae.

Asili ya mti huu ni Uhindi lakini sikuhizi upandwa mahali pengi pa kanda za tropiki na nusutropiki.

Hutumika kwa 

kulisha mifugo, chakula cha watu,kuboresha mashamba, kusafisha maji ya kunywamitishamba. 

Majani yake ni chakula bora (mboga chungu), lakini maganda mabichi, maua, mbegu, mafuta ya mbegu na mizizi hulika pia.

Watafiti wa sayansi na tiba wamegundua kuwa mti huitwa mlonge ambao kwa Kiingereza unaitwa Moringa Oleifera una uwezo wa kutibu maradhi mengi katika mwili wa mwanadamu

Nimesikia mengi kuhusiana na mti wa Mlonge lakini hii ni kali zaidi CAPE TOWN, (IPS).
Wakati tatizo linalipolikabili Bara la Afrika, watu wanaangalia uwezekano wa kupata misaada kutoka kwenye mashirika ya kimataifa kutoka nje ya bara hilo.

Lakini hali ya ukame inayoongezeka kwa kasi, miti yenye kuhimili ukame huku ikiwa na majani yenye viini lishe vingi inaweza kuwasaidia watu maskini, pia maeneo ya usalama wa chakula na utapiamlo, wao wenyewe.

Shamba lenye hekta 15 lilipandwa miti ya Mlonge au wengine huuita mti wa miujiza ambao kwa Kiingereza unaitwa Moringa Oleifera, tayari umeshaanza kuleta mabadiliko katika jimbo moja maskini zaidi la Afrika Kusini la Limpopo.

Majani ya Mlonge yamepachikwa jina la chakula chenye viwango kwasababu wanasayansi waligundua yana kiasi cha madini ya 

Kalisium yanayoweza kupatiakana katika glasi nne za maziwa, kiasi cha vitamini c inayopatikana kwenye machungwa saba, Potasium ya kwenye ndizi mbivu tatu. Pia unapata kiasi cha madini ya chuma mara nne zaidi.

KAMA kuna mti wenye faida nyingi za kiafya, basi Mlonge unaweza kuwa unaongoza.

Kila eneo la mti huu, kuanzia majani, maua, mbegu, magamba hadi mizizi yake ina virutubisho vya kipekee vyenye faida nyingi za kiafya kwa binadamu.

Majani ya Mlonge yanaweza 

kutafunwa mabichi, yaliyochemshwa kama mboga au yaliyokaushwa na kusagwa kuwa unga. 

Unga wake unaweza kuhifadhiwa kwa miezi kadhaa bila kupoteza ubora na faida zake za kiafya.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na shirika moja lijulikanalo kama Trees For Life,
These tiny leaves could save millions of lives.

Majani ya Mlonge yana 

Vitamin A nyingi kuliko karoti, vitamin C nyingi kuliko machungwamadini ya Potassium nyingi kuliko ndizi mbivu, halikadhalika ubora wa protini yake ni bora kushinda maziwa na mayai.

Kutokana na kuwa na kiasi kingi cha 

madini ya chuma (Iron), kasiamu (Calcium) na vitamin nyingi za aina mbalimbali, majani ya mmea huu yamekuwa yakitumika kama ‘tonic’ kwa watoto wadogo na vijana ili kuimarisha mifupa na kusafisha mfumo wa damu mwilini.

Ili kutengeneza ‘tonic’, 

saga majani mabichi ya Mlonge pamoja na maji, yachuje kisha changanya na maziwa halisi. 

Inaelezwa kuwa juisi ya aina hii ni dawa nzuri kwa waja wazito, kwani

huboresha njia ya uzazi na kumuwezesha mama kuzaa bila matatizo na kuondoa matatizo baada ya kujifungua. 

Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali, mti wa Mlonge unatibu karibu magonjwa 300 ya aina mbalimbali, yakiwemo yale magonjwa sugu, baadhi yake ni kama haya yafuatayo:

Mlonge unaweza kutibu 

Pumu, KikohoziKifua Kikuu.

 Aidha, magonjwa mengine kama 

Kisukari, Shinikizo la damu (la juu na chini), magonjwa ya ngozi, magonjwa ya kwenye njia ya mkojo (UTI) kuongeza kinga ya mwili (CD4)kuongeza nguvu za kiume

FAIDA ZA MBEGU ZA MLONGE
Mbegu za Mlonge hutibu maradhi pia kama 

Malaria, Saratani ya tumbo, hupunguza sonona stress,huleta hamu ya kunywa maji, jambo amabalo ni adimu kwa watu wengi

Mbegu hizo za mti huo wa ajabu bado zinahamasisha jamii kuamka na kuutambua umuhimu wa mti MLONGE kwa mbegu hizo hutoa 

mafuta ya kupikia pamoja na mafuta ya kujipaka mewilini kwa nyakati tofauti.

Kwa upande wa mafuta ya kupikia chakula wataalam anasema mafuta yake ya kupikia 

huua sumu kwenye chakula yaani Bacteria na huondoa cholesterol. 
Mafuta ya kupaka mwilini yaani (Moringa Skin Care Oil).

Mlonge unaendelea kutoa faida kemkem kwa mtanzania na jamii yote duniani kwani umeweza kuwapendelea na wanamichezo kwa kutoa mafuta ambayo  yanachua pindi mchezaji anapokuwa ameshikwa na misuli wakati akiwa anacheza,

wataalam wanaainisha kwamba katika utafiti wamefanikiwa kutambua faida nyingine ya matumizi ya mti huo baada ya kufanikiwa kutengeneza mafuta ya kuchua na kuondoa maumivu yatokanayo na kukaza kwa misuli ya mwili yaani (MORINGA MASSEGE OIL)ambayo

huondoa maumivu ya mgongo, kiuno, miguu, hutibu baridi, na hupasha misuli joto

Maganda(magome) ya Mlonge husaidia 

kusafisha maji(water treatment).

Mizizi hutumika kutibu watu walio na 

malaria sugu au watu wanaopata homa ya usiku au wanaotiririka sana jasho wakati wa homa. 
Mizizi hutumika kwa kusaga unga wake na kutumia kijiko cha chai mara tatu kwa siku.

Tumia mbegu 3x3 muhimu kila ukitafuna mbegu tatu kumbuka kutumia maji glass 3 au zaidi)

Ndugu tuna tabibu mbalimbali, za asili na zisizo na madhara kama ya vidonge vya makemikali na bado tunapuuza.

TIBA NA MBOLEA KWA MIMEA
Watafiti pia wamegudua kuwa majani ya mti wa mlinge yanaweza kutumika kama mboea shambani kwa mimea ya aina zote kutokana na viinilishe na virutubisho vilivyomo katika mmea huu,lakini pia

mizizi yake inapotambaa huambukiza virutubisho kwa mimia iliyo jirani katika eneo la mita tano za mraba ulikopandwa mti wa mlonge.

Sunday, March 12, 2017

TIBA YA ALOEVERA

Bila shaka anaufahamu mmea huu, kwani umechukulia umaarufu miaka ya hivi karibuni katika kutibu magonjwa mbalimbali. Japo mmea huu ni miongoni mwa mimea ambayo ni michungu sana hasa ambapo unatumia. Lakini uchungu huo ndio dawa yenyewe.  Lakini wataalamu mbalimbali wanasema ya kwamba ili kuondokana na uchungu huo wanashauri uweze kuchanganya na asali mbichi ambayo hajachakachuliwa.

Ifuatavyo ndiyo kazi ya mmea wa aloe vera katika kutibu magonjwa yafuatayo:

Huondoa sumu mwilini na kufanya utendaji kazi wa mwili urudi katika hali ya kawaida.Haidia kujenga seli mpya baada ya majeraha ya moto, kujikata, michubuko,Aloe beta husaidia kutibu vidonda vya tumbo.Husaidia matatizo ya kutopata haja, pia maumivu wakati wa haja kubwa na ndogo.Huondoa matatizo ya ngozi kama chunusi (acne) na fangasi.Ni msaada tosha katika umeng’enyaji wa chakula.kuongeza kinga ya mwili dhidi ya mogonjwa mbalimbali.Mmea huu husaidia pia kuondoa maumivu sehemu mbalimbali za mwili, pia husaidia kupunguza uchovu kwa kiwango cha hali ya juu sana.Hutibu matatizo ya kuhara na kutopata haja kubwa kiurahisi.Lakini vilevile aloe vera husaidia wanaume wengi ambao wanaosumbuliwa na matatizo ya kuziba kibofu cha mkojo na pia kinamama wanao sumbuliwa na uambukizi kwenye njia ya mkojo (UTI).

Namna ya kuandaa mchanganyiko wa aloevera.

katakata vipande vidogovidogo kisha viweke katika maji safi na salama, kisha  subiri mchanganyiko huu kwa muda wa saa moja kisha anza kwa ajili ya matibabu.

Ili kupunguza uchungu, unaweza kutengeneza juisi yake na kuichanganya na asali ya nyuki wadogo.

Matumizi:

Kunywa kila siku kwa muda wa wiki mbili, asubuhi na jioni kabla ya kula chochote. Kwa kutumia kikombe kimoja cha chai. 

HISTORIA YA BOB MARLEY

Alikataa kuandika urithi kwa kuamini kuwa marastafari huwa hawafi.

Robert Nesta Marley,ambaye baadaye alikuja kujulikana kama Bob Marley,alizaliwa Februari 6,1945 katika kijiji cha Nine Mile kwenye Parishi ys mtakatifu Ann huko Jamaica.

Baba yake Norval Sinclair Marley alikuwa mzungu na mama yake Cedelia Booker alikuwa Mjamaica mweusi.

Historia ya maisha yake haitofautiani sana na wanamuziki wenzake wa reggae Peter Tosh aliyelelewa na shangazi yake na Bunny Wailer aliyelelewa na baba yake zaidi,ni historia ya huzuni iliyo muacha Bob Marley chini ya mzazi mmoja(mama yake) pale alipofiwa na baba yake akiwa na umri wa miaka kumi tu.

Norval Sinclair (baba yake Bob Marley) alikuwa nahodha wa meli na muangalizi wa mashamba,alikufa mwak 1955 akiwa safarini,wakati huo alikuwa na umri wa miaka 60.

Kifo hicho kilimfanya mama yake Bob Markey ahamishe makazi kwenye mji wa Kingston,huko Bob alikutana na Bunny Wailer wakawa marafiki na kujifunza muziki pamoja.Akiwa na umri wa miaka 14,

Bob Marley aliacha shule na kujiunga na chuo cha ufundi wa kuchomelea vyuma,muda wakewa kupumzika alikuwa na Bunny Wailer kwenye muziki,kipindi hiko mwalimu wao alikuwa Joe Higgs,

Muimbaji wa mtaani mwenye imani ya kirastafari.Chini ya Joe Higgs walikutana na Peter Tosh na kuungana naye.

Mwaka 1962 Bob Marley alirekodi nyimbo zake mbili za kwanza ambazo ni;"Usihukumu"(judge not) na "kikombe kimoja cha chai"(one cup of tea) chini ya muandaaji Leslie Kong,

lakini nyimbo hizo hazikukubalika sana.Mwaka 1963 akashirikiana na Bunny Wailer,Peter Macintosh(Peter Tosh),Junior Braithwaite,Beverly Kelso na cherry Smith n kuunda kundi la "The Teenagers" kundi hilo lilijibadili majina na kuwa "The wailing rude boys","The wailling wailers" na mwishowe "The wailers".

Mwaka 1964 na 1965 watoa vibao vikali kama "Usiwe na wasiwasi"(simmer down) na "Nafsi isiyokubali"(soul rebel)nyimbo hizi zilikonga nyoyo za Wajamaika wengi

Hata hivyo kufikia mwaka 1965 lilibakiwa na wakali watatu tu,yaani Bob Marley,Bunny Wailer n Peter Tosh,baada ya wengine kujiengua.

Mwaka 1966 Bob Marley alimuoa kimwana Rita Anderson na kwenda kuishi kwa muda na mama yake huko Wilmington,Delaware nchini Marekani..

 Na kuibuka na imani kali ya kirastafari na kuja na mtindo wa kufuga nywele uitwao "dreadlocks".

Baada ya hapo Bob Marley na kundi lake la The wailers walitoa vibao kemkem vilivyoitikisa Dunia.

Kati ya vibao hivyo ni;Africa unit,Zimbabwe,Could oyu loved?,Iron lion zion,Is this love,Buffalo soldier na vingine vingi.

Huyo ni Bob Marley,mfalme wa reggae aliyepinga ubaguzi kwani hata yeye mwenyewe alisema "Wananiita chotara,lakini mimi siegamii upande wowote bali nipo upande wa Mungu aliye niumba kutoka kwa weusi na weupe".

Hiyo ni biograph ya mwanaharakati huyo wakupinga ubaguzi."REST IN PEACE RASTAFARAE"

Saturday, March 11, 2017

TAmbua siri ya herufi ya mwanzo katika jina lako

Siri ya herufi ya mwanzo ya Jina lako

Je Unajua Siri ya herufi ya mwanzo ya jina lako?. Soma hapa utaweza kuelewa Tabia zako au tabia za rafiki au mpenzi wako.

>HERUFI A
>Mwenye jina linaloanziana na herufi A ni mtu anayependa mambo makubwa, anajiamini na mwenye uwezo wa kutimiza malengo yake. Ni mtu mwenye tahadhari, mchangamfu na mpenda matukio. Anapenda Kuheshimiwa, anapenda Mamlaka, na ana kiburi, na hasira. Herufi A inawakilisha Nyota ya Punda.
>HERUFI B
>Mwenye jina linaloanziana na herufi B ni mtu, mkarimu, muaminifu, na hupenda kazi. Ni Jasiri, shujaa na mkatili katika vita au pale anapotaka kulinda vilivyo katika himaya yake. Herufi B inawakilisha Nyota ya Ngombe,
>HERUFI C
>Mwenye jina linaloanziana na herufi C ni mtu wa kukubadilika badilika, mshindani na hupenda kupigania malengo yao wanayopenda. Ni watu wa wabunifu na wanaopenda mawasiliano Herufi C inawakilisha Nyota ya Mapacha,
>HERUFI D
>Mwenye jina linaloanziana na herufi D ni mtu anayependa usawa, Biashara. Ni watu wanaopenda kuamrisha na mwenye kupenda usafi. Ni jeuri na wenye msimamo. Herufi C inawakilisha Nyota ya Kaa,
>HERUFI E
>Mwenye jina linaloanzia na herufi E ni mtu mwenye roho nzuri ,yenye mapenzi na huruma. mwenye kupenda uhuru katika mapenzi na mchangamfu. Kinyume na hivyo atakuwa ni mtu asiotegemewa na kigeugeu. Herufi E inawakilisha Nyota ya Simba,
>
>HERUFI F
>Mwenye jina linaloanzia na herufi F ni mtu mwenye mapenzi,huruma , roho nzuri na ana uwezo wa kuwafariji watu. Ni mtetezi wa watu na mwenye huzuni lakini ni mzito wa kufanya maamuzi. Herufi F inawakilisha Nyota ya Mashuke,
>HERUFI G
>Mwenye jina linaloanzia na herufi G ni mtu mwenye mwenye imani ya kidini na nguvu za kiroho. Ana kipaji cha kubuni na uwezo wa kutatua matatizo ya watu. ni mtu mwenye hisia kali,msomi, mpweke na mkaidi wa kukubali ushauri wa kutoka kwa watu. Herufi G inawakilisha Nyota ya Mizani,
>HERUFI H
>Mwenye jina linaloanzia na herufi H ni mtu mwenye ubunifu na nguvu katika biashara, hupata faida kubwa kutokana na jitihada na bidii zake. ni mwenye mawazo mengi, mchoyo na mbinafsi. Herufi H inawakilisha Nyota ya Nge,
>HERUFI I
>Mwenye jina linaloanzia na herufi I ni mtu mwenye kupenda sheria, ana huruma na utu. Wakati mwingi hajiamini na ni mwenye hasira za haraka. Herufi I inawakilisha Nyota ya Mshale,
>HERUFI J
>Mwenye jina linaloanzia na herufi J ni mtu mwenye matamanio,mkweli, mkarimu na muerevu. asiyekubali kushindwa na hupata mafanikio makubwa. Wakati mwingine anakuwa ni mtu mvivu na aliyekosa mwelekeo. Herufi J inawakilisha Nyota ya Mbuzi,
>HERUFI K
>Mwenye jina linaloanzia na herufi K ni mtu mwenye jeuri. mwenye msimamo thabiti,mashuhuri na mwenye uwezo wa kushawishi na kuamsha hisia za watu wana uwezo wa utambuzi ambao watu wengi hawana. ni mtu asioridhika na hali ya kimaisha. Herufi K inawakilisha Nyota ya Ndoo,
>HERUFI L
>Mwenye jina linaloanzia na herufi L ni mtu wa vitendo, mwenye hisani na aliyejipanga vizuri kimaisha. Huwa wanapata ajali mara kwa mara. Herufi L inawakilisha Nyota ya Samaki,
>HERUFI M
>Mwenye jina linaloanzia na herufi M ni mtu mwenye kujiamini sana, mchapakazi na hupata mafanikio. ni mtu mropokaji,mwenye haraka na mwepesi kukasirika. Herufi M inawakilisha Nyota ya Punda
>HERUFI N
>Mwenye jina linaloanzia na herufi N ni mtu mwenye ubunifu, hisia kali na hupenda kuwasiliana lakini ana wivu sana. Herufi N inawakilisha Nyota ya Ngombe
>
>HERUFI O
>Mwenye jina linaloanzia na herufi O ni mtu mwenye subra, mvumilivu na mwenye bidii ya kusoma. Ni mtu mwenye kupenda kutumikia jamii na mwenye uwezo mkubwa wa kudhibiti hisia. Herufi O inawakilisha Nyota ya Mapacha
>HERUFI P
>Mwenye jina linaloanzia na herufi P ni mtu mwenye uwezo wa kuamrisha na hekima kubwa. Ana nguvu za kiroho lakini anapenda sana kujitumbukiza kwenye mambo ya watu. Herufi P inawakilisha Nyota ya Kaa
>HERUFI Q
>Mwenye jina linaloanzia na herufi Q ni mtu mwenye kupenda mambo ya asili. Ni watu wasiyoelezeka nawana uwezo wa kuonyesha vitu visivyojulikana hata hivyo ni mtu aliyepooza sana. Herufi Q inawakilisha Nyota ya Simba
>HERUFI R
>Mwenye jina linaloanzia na herufi R ni mtu mwenye uvumilivu, wenye huruma lakini ana hasira za haraka. Muda wote anakuwa mpenda amani. Herufi R inawakilisha Nyota ya Mashuke
>HERUFI S
>Mwenye jina linaloanzia na herufi S ni mtu mwenye mvuto mkali wa kuleta utajiri. Ni watu wenye maamuzi ya ghafla na hupenda mageuzi makubwa. Herufi S inawakilisha Nyota ya Mizani
>HERUFI T
>Mwenye jina linaloanzia na herufi T ni mtu mwenye kupenda ushauri wa kiroho, anatumia nguvu za ziada kusaidia watu na hupata mafanikio baada ya muda mrefu. Ni watu wenye hisia kali sana na ni wepesi kushawishika. Herufi S inawakilisha Nyota ya Nge
>HERUFI U
>Mwenye jina linaloanzia na herufi U ni mtu mwenye bahati kubwa kwa ujumla. Anapenda uhuru katika mapenzi. Lakini ni mtu mbinafsi, mwenye tamaa na aliyekosa maamuzi. Herufi U inawakilisha Nyota ya Mshale.
>HERUFI V
>Mwenye jina linaloanzia na herufi V ni mtu Mchapakazi, wenye bidii na asie choka. Hata hivyo ni watu wasiotabirika. Herufi U inawakilisha Nyota ya Mbuzi.
>HERUFI W
>Mwenye jina linaloanzia na herufi W ni mtu muwazi, wachangamfuu kupita kiasi na mwenye uwezo wa kutambua mtu mwema na mbaya. Ni watu wenye tamaa na hufanya mambo ya hatari. Herufi W inawakilisha Nyota ya Ndoo.
>HERUFI X
>Mwenye jina linaloanzia na herufi X ni mtu asiyependa kuwekewa vizuizi katika kwenye anasa na ni rahisi kujiingiza kwenye uzinzi na kujitoa uaminifu. Herufi X inawakilisha Nyota ya Samaki.
>HERUFI Y (YASINTA)
>Mwenye jina linaloanzia na herufi Y ni mtu mwenye kupenda Uhuru na hawapendi kupingwa jambo lao lolote. Ni watu wanaokosa uamuzi na husababishia kupoteza bahati katika maisha. Herufi Y inawakilisha Nyota ya Punda
>HERUFI Z
>Mwenye jina linaloanzia na herufi Z ni mtu mwenye kupenda matumaini na amani. Ni wenye msimamo mkali ila wanashauriwa kufikiria kabla ya kuamua jambo. Herufi Z inawakilisha Nyota ya Ngombe.