Friday, March 24, 2017

TIBA TOSHA YA MBEGU ZA MABOGA

Watu wengi hupenda zaidi ya kula boga kuliko mbegu zake. Wengi hufanya hivi kwa sababu huona hazina faida kwa kuwa wanavutiwa na boga zaidi, hii sawa nakusema watu hupenda zaidi mnofu kuliko kula mifupa, lakini ukweli ni kwamba mbegu za maboga ni za muhimu sana kwani zina wingi protini na madini ya kutosha ambayo ni muhimu sana katika miili yetu.

Madini ambayo yanapatikana katika mbegu za maboga kama vile zinki, kopa, maginizia, manganizi na chuma. Tafiti mbalimbali zimethibitisha pasipo na shaka kuwa mbegu za maboga zina faida nyingi kiafya na zina uwezo wa kukuepusha na magonjwa hatari zaidi ya 10  na magonjwa hayo ni kama:

1.Magonjwa ya moyo.
Kiasi kingi cha madini ya magnesium katika mbegu za maboga yanazifanya mbegu hizi kuwa muhimu sana kwa watu wenye magonjwa mbalimabli ya moyo. Madini ya magnesium ni muhimu kwa ajili ya kuimarisha msukumo wa damu kwenye moyo na kuimarisha afya ya mishipa ya damu hatimaye kutibu na kuzuia magonjwa ya moyo.

2. Husaidia uzalishaji wa maziwa kwa wingi kwa kina mama wanaonyonyesha.
Hivyo kwa mama anenyonyesha anashauriwa kutumia  mbegu za maboga kwa wingi ili kuzalisha maziwa kwa wingi.

3. Huongeza uwezo wa macho kuuona vizuri.
Mbegu za maboga zina Vitamini E, vitamini A, lutein, beta-carotene na zeaxanthin, vitu hivi vinavyopatikana katika mbegu za maboga ni mhimu kwa ajili ya nuru ya macho. Vitamini A na madini ya zinki ni mhimu kwa ajili ya uzalishaji wa ‘melanin’ kimeng’enya mhimu ambacho hutengenezwa kwa asili na miili yetu kwa ajili ya ulinzi wa afya ya macho.

4.Husaidia kuondokana na matatizo ya unene unaotokana na wingi wa mafuta ( cholestrol) mwilini.

5.huondoa harufu mbaya ya kinywa na husaidia pia wenye tatizo la kufunga choo au kupata choo

6.Husaidia kurekebisha sukari mwilini na kuwezesha kongosho kufanya kazi yake vizuri.

7. Huondoa sumu mbalimbali mwilini na hasa kwenye figo.

8.Husaidia kuondoa shinikizo la damu.

9. Ni kinga dhidi ya kansa ya kizazi kwa wanaume na wanawake.

10. Huboresha akili na kumbukumbu kwa watoto na watu wazima ( kazi ya zinc na omega 3 Fatty).

Hivyo kila wakati inashauriwa kutafuna mbegu hizi zikiwa mbichi kuliko zikiwa zimechemshwa au kukaangwa,  kwani ukitumia ambazo zimechemshwa au kukaangwa kuna uwezekano mkubwa wa kupoteza baadhi ya vitamini.

No comments:

Post a Comment