Monday, March 20, 2017

FAIDA YA TANGAWIZ KIAFYA

Asante kwa kuendelea kutembelea Mbinuzamafanikio.blogspot.com, kwani tunaamini ya kwamba unaimarika sana kifkra kupitia makala hizi. 

ambo la msingi katika makala ambazo unazisoma kupitia ukurasa huu unatakiwa kuchukua hatua, hii itakuwa njia bora zaidi la kuweza kutimiza lile kusudio lako.

Tukiachana na hayo naomba nikukaribishe katika Makala haya, kwani siku ya leo tutazungumzia umuhimu wa tangawizi katika kutibu magonjwa mbalimbali. Kwani naamini kila mmoja wetu anaifahamu vyema tangawizi.

Zifuatazo ndizo faida za tangawizi.

1. Tangawizi hutibu matatizo ya koo pamoja na kukauka kwa sauti.

Unachotakiwa kufanya ni:
Tafuna vipande vidogo vya Tangawizi.

2. Tangawizi huzuia kichefuchefu na kutapika.

Unachotakiwa kufanya:
Kunywa mchanganyiko wa Juice ya Tangawizi.

3.Husaidia kutibu maumivu makali ya tumbo.

Unachotakiwa kufanya ni :
Changanya kijiko kimoja cha au viwili vya Tangawizi iliyosagwa na kijiko kimoja au viwili vya mafuta ya Kastoli. Kunywa kijiko kimoja mara mbili kwa siku.

4.Tangawizi husaidia kwa kiwango kikubwa matitizo ya kuuma kwa meno pia husaidia kutibu maumivu ya kichwa.

Unachotakiwa kufanya ni:
Chukua Tangawizi ya Unga koroga na maji kidogo iwe nzito kama tope. Jipake na uchue kwenye paji lako la uso kabla ya kulala. Kwa Jino jipake na uchuwe kwenye Shavu.

6. Hutibu mafua makali na kikohozi, osha na kisha

Unachotakiwa kufanya ni :
Twanga tangawizi na uichemshe katika maji kwa muda mrefu.
Unaweza kuweka majani ya chai au maziwa na kisha kunywa taratibu ikiwa ya moto. Fanya hivyo kwa siku mbili na mafua yatapona kabisa.

Lakini kabla akaweka nukta matumizi mengine ya  tangawizi ni kurekebisha matumizi ya kina mama katika zile siku ngumu. Mathalani, iwapo tarehe zinabadilika mara kwa mara unaweza kutumia kurekebisha mwenendo wa siku hizo muhimu.

No comments:

Post a Comment