Thursday, March 9, 2017

HISTORIA YA EDWARD SOKOINE

Edward Moringe Sokoine, 4 Oktoba 1983

Tarehe kama ya leo 12.04.1984, Taifa la Tanzania lilimpoteza kiongozi wake shupavu, aliyekuwa Waziri Mkuu Hayati Edward Moringe Sokoine, kufuatia ajali ya gari eneo la WAMI-DAKAWA Kilomita 35 nje kidogo ya mji wa Morogoro. Waziri Mkuu huyu alikuwa akitokea Dodoma kuelekea Dar es Salaam baada ya kufunga Kikao cha Bunge mjini Dodoma.

Baada ya kuagwa kiserikali Jijini Dar, marehemu Sokoine alisafirishwa kwenda Monduli Juu Arusha kwa mazishi. 

Atakumbukwa kama kiongozi shupavu na ambaye alikuwa hacheleweshi utekel;ezaji wa jambo pale linapoonekana linatakiwa utekelezaji wa haraka na madhubuti. Alipigana kupunguza rushwa na ufujaji wa mali, pia ulimimbikizaji wa mali mikononi mwa wachache (Ufisadi).

Mengine zaidi..

Edward Moringe Sokoine alizaliwa tarehe 1 Agosti 1938 alikuwa Waziri  Mkuu wa Tanzania tarehe 13 Februari 1977 hadi tarehe 7 Novemba  1980 tena akawa Waziri mkuu toka tarehe 24 February hadi tarehe  12 Aprili 1984. 

Alikuwa ni mtu aliyepanda usawa kwa kila mtu aliamini  kila mtu anaweza kuwa na maendeleo kama akijituma katika kilimo  na sehemu alipo pamoja na kujitegemea akiwa ni wakala wa  mabadiliko katika nchi, mtu asielaumu na mwaminifu. 

Alizaliwa Monduli Mkoani Arusha Tanzania,  alipata elimu  ya msingi na sekondari katika miji ya Monduli na Umbwe toka mwaka  1948 hadi 1958.

Mwaka 1961 alijiunga na chama cha TANU  baada ya kuchukua masomo katika Uongozi nchini Ujerumani 1962  hadi mwaka 1963.

Aliporudi kutoka Ujerumani alikuwa Afisa Mtendaji  wa Wilaya ya Masai, tena akachaguliwa kuwa mwakilishi wa jimbo  la Masai. 

Mwaka 1967 alikuwa naibu waziri wa mawasiliano, usafiri  na kazi. Hatua nyingine katika maisha yake alijitangaza  mpaka kuwa Waziri Mkuu 1970. 

Mwaka 1972 aliamia kwenye Waziri wa usalama. Mwaka 1975  alichaguliwa kwenye Bunge tena wakati huu kupitia Monduli.  

Miaka miwili baadae akawa mjumbe wa Kamati kuu ya Chama Cha  Mapinduzi (CCM), 1977 alianza muhula wa kwanza ofisini akiwa  Waziri Mkuu wa Jamuhuri wa Muungano wa Tanzania. 

Muhula huu  ulidumu hadi 1981, baada ya kutulia kwa kipindi cha mwaka alikuwa  tena Waziri Mkuu tena mwaka 1983, alikaa mwaka mmoja ofisini  mpaka alipofariki Aprili 1984 kwa ajali ya gari. 

Kuna Chuo Morogoro  Tanzania kinaitwa jina lake (Sokoine University Of Agriculture (SUA)  kilianza mwaka 1984 kama chuo cha kilimo kinachotoa diploma  katika kilimo. Chuo hicho kikaongezwa hadi kutoa mchepuo wa  kilimo mwaka 1969 chini ya Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam.

BAADHI YA KAULI ZA SOKOINE

“Ole wake kiongozi mzembe na asiye na nidhamu nitakayemkuta: Kiongozi wa siasa hana usalama wa aina yoyote. Usalama wake ni kudra ya Mungu na Wananchi peke yake. Viongozi wazembe na wabadhirifu wahesabu siku zao. Labda tusiwajue. Hawa hatuna sababu ya kuwapa imani, kuwa tutawalinda kama vitendo vyao viovu” – Edward Moringe Sokoine, 26 Machi 1983

“Wajibu wa kila Mtanzania, kila familia na kila anayekula ni kujilisha mwenyewe. Si wajibu wa Taifa kumlisha mtu. Unaweza ukasaidiwa unapopatikana na janga. Lakini kama hakuna janga ni wajibu wa kila mtu aweze kujitosheleza kwa chakula na atoe ziada kwa Taifa” – 

No comments:

Post a Comment